Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Yeremia 1:9 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

9 Kisha Yawe akanyoosha mukono wake, akagusa kinywa changu, akaniambia: Nimetia maneno yangu ndani ya kinywa chako.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Yeremia 1:9
22 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Alifanya maneno yangu kuwa makali kama upanga mukali, alinificha katika kivuli cha mukono wake; aliufanya ujumbe wangu kuwa mukali kama chongo ya mushale, akanificha kama mushale ndani ya mufuko wake.


Bwana wetu Yawe amenifundisha jinsi ya kusema, kusudi niwatie moyo wale waliochoka. Kila asubui ananipa hamu ya kusikiliza mambo anayotaka kunifundisha.


Nimeyaweka maneno yangu katika kinywa chako; nimekuficha katika kivuli cha mukono wangu. Mimi nilizitandaza mbingu, nikaiweka misingi ya dunia. Mimi ninawaambia, enyi watu wa Sayuni: Ninyi ni watu wangu.


Yawe anasema: Mimi ninafanya nanyi agano hili: Roho wangu anayekuwa juu yenu, maneno niliyoyaweka katika kinywa chenu, hayataondoka kwenu hata kidogo, wala kwa watoto na wajukuu wenu, tangu sasa na hata milele.


Basi, Yawe akasema hivi: Kama ukinirudilia, nitakurudisha katika hali yako ya mbele, nawe utanitumikia tena. Kama ukisema maneno ya maana, yasiyokuwa ya upuuzi, basi utakuwa musemaji wangu. Watu watakufikia wewe, wala si wewe utakayehitaji kuwaendea.


Kisha, nabii Yeremia akamwelezea Zedekia, mufalme wa Yuda, maneno hayo yote huko Yerusalema,


Twaa kizingo cha kitabu uandike humo maneno yote niliyokuambia juu ya Israeli, juu ya Yuda na mataifa yote, tangu siku nilipoanza kusema nawe, wakati Yosia alipokuwa mufalme mpaka leo.


Yawe wa majeshi anasema hivi: Kwa sababu wao wamesema jambo hilo, sasa nitayafanya maneno niliyokupa wewe Yeremia kuwa moto. Nao watu hawa watakuwa kuni, na moto huo utawateketeza.


Tena akaniambia hivi: Wewe mwanadamu, maneno yote nitakayokuambia uyaweke ndani ya moyo wako, na uyasikilize vizuri.


Hapo, mukono ukanigusa, ukanisimamisha, na kuimarisha miguu na mikono yangu.


Kisha, kiumbe kimoja chenye umbo la mutu, kiliigusa midomo yangu, nami nilifungua midomo yangu na kumwambia huyo aliyesimama karibu nami: Ee bwana, maono haya yameniletea maumivu makali hata nimeishiwa nguvu.


Yawe akamupa Balamu maneno atakayosema na kumwambia arudi kwa Balaki.


Lakini watakapowapeleka kwa kuhukumiwa, musijihangaishe juu ya maneno mutakayoyasema wala juu ya namna mutakavyosema, kwa maana saa ile ile mutapewa maneno mutakayoyasema.


Basi Yesu akamwondoa yule mutu kati ya kundi, akaenda naye mbali kidogo, akamutia vidole ndani ya masikio, akatema mate na kumugusa ulimi kwa mate yale.


kwa sababu Roho Mutakatifu atawafundisha saa ile ile maneno munayopaswa kusema.”


Kwa maana mimi mwenyewe nitawapa masemi na hekima hata waadui zenu hawataweza kuyapinga wala kuyakataa.


Hicho ndicho mulichomwomba Yawe, Mungu wenu, kule Horebu, siku ile mulipokusanyika na kusema: ‘Tusisikie tena sauti ya Yawe, Mungu wetu, wala tusiuone tena moto huu mukubwa, kusudi tusikufe!’


Nitawachagulia kati ya wandugu zao wenyewe nabii kama wewe, nitatia maneno yangu ndani ya kinywa chake, naye atawaambia yote nitakayomwamuru.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ