Lakini Musa akamwambia Yawe: “Angalia, Waisraeli hawanisikilizi mimi. Namna gani mufalme wa Misri atanisikia! Tena mimi ni mutu asiyekuwa na ujuzi wa kuongea!”
Basi, mimi nikasema: Ole kwangu! Mimi nimeangamia, maana, midomo yangu ni michafu, na watu ninaoishi nao ni wenye midomo michafu. Hata hivyo, kwa macho yangu mwenyewe, nimemwona Mufalme, Yawe wa majeshi.
Kisha mimi nikasema: Ee Bwana wangu Yawe! Manabii wanawaambia watu hawa kwamba hakutakuwa vita wala njaa, kwa sababu umeahidi kwamba kutakuwa tu amani katika inchi hii.
Kisha nikasema: Ee, Bwana wangu Yawe, hakika umewadanganya kabisa watu hawa, nao Yerusalema! Uliwaambia mambo yataongoka vizuri kwao, kumbe maisha yao yako katika hatari kabisa!
Halafu nikamwambia hivi: Ee, Bwana wangu Yawe, sijajichafua hata kidogo kwa kula nyamafu wala nyama aliyeuawa na nyama wa pori, wala sijapata kuonja nyama anayehesabiwa kuwa muchafu tangu ujana wangu.
Nami nikauliza: Watu hawa wanakuja kufanya nini? Yeye akanijibu: Watu hawa wamekuja kuyatisha na kuyaangamiza yale mataifa yenye nguvu ambayo yaliishambulia inchi ya Yuda na kuwatawanya watu wake.