Mambo haya yote yaliwafikia kusudi yakuwe mufano kwa watu wengine; yameandikwa kwa kutuonya sisi, kwa maana tunaishi katika kipindi cha mwisho wa nyakati.
Kwa hiyo musihukumu mutu mbele ya wakati uliopangwa; mungojee mpaka Bwana atakaporudia. Yeye ndiye atakayeonyesha wazi katika mwangaza mambo yote yaliyofichwa katika giza na kufunua nia za siri za watu. Halafu kila mutu atapokea sifa anayostahili toka kwa Mungu.
Wandugu, musisemeane ubaya. Yule anayesema ubaya juu ya ndugu yake au kumuhukumu, anasema ubaya juu ya Sheria na kuihukumu. Ukihukumu Sheria, wewe si mwenye kutii Sheria, lakini mwenye kuihukumu.
Mungu peke yake ndiye anayesimamisha Sheria na anayeweza kuhukumu. Ni yeye peke yake anayeweza kuokoa na kuangamiza. Basi wewe unayemuhukumu mwenzako, unajizania kuwa nani?
Basi wandugu, muvumilie mpaka Bwana atakaporudia. Muangalie namna mulimaji anavyongojea shamba litoe mavuno yanayokuwa ya faida kubwa. Yeye anavumilia mpaka wakati mvua ya kwanza na ya mwisho zinaponyesha.
Sikiliza, ninasimama kwenye mulango na ninapiga hodi. Kama mutu akisikia sauti yangu na kunifungulia, nitaingia kwake, nami nitakula pamoja naye, na yeye atakula pamoja nami.