Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Yakobo 5:4 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

4 Ninyi hamukulipa mishahara ya watumishi waliotumika katika mashamba yenu. Musikilize mashitaki yao! Malalamiko ya wavunaji yamefika katika masikio ya Bwana Mwenye Uwezo!

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Yakobo 5:4
23 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Yawe akasema: “Umefanya nini? Damu ya ndugu yako inanililia kutoka katika udongo.


Hata wakasababisha kilio cha wamasikini kimufikie Mungu. Mungu akasikiliza kilio cha wale walioteswa.


Yeye ni kama mutumwa anayetamani kivuli, kama mutumishi anayengoja kwa hamu mushahara wake.


Mumwimbie sifa Yawe anayekaa Sayuni! Muyatangazie mataifa mambo aliyotenda!


Usimutukane Mungu, wala kumulaani mukubwa wa watu wako.


Hakika, kilio cha Waisraeli kimenifikia; nimeona jinsi Wamisri wanavyowatesa.


Yawe wa majeshi asingetuachia watu wachache, tungekwisha kuwa kama watu wa Sodoma tungekuwa na hali ileile ya Gomora.


Shamba la mizabibu la Yawe wa majeshi ni taifa la Waisraeli, na mizabibu mizuri aliyoipanda ni watu wa Yuda. Yeye alitazamia watu wafuate sheria yake, akaona mauaji; alitazamia haki, alisikia kilio!


Nimemusikia Yawe wa majeshi akisema hivi: Hakika nyumba nyingi zitabaki tupu, zile kubwa na nzuri zitabaki wazi bila wakaaji.


Ole kwako Yoyakimu, wewe unayejijengea nyumba kwa njia isiyokuwa ya haki, na kuiwekea magorofi kwa njia isiyofuata sheria ya Mungu. Unayewatumikisha watu bure pasipo kuwalipa mishahara yao.


Usimutese mwenzako wala kumwibia. Usikae na mushahara wa mutumishi wako usiku kucha mpaka asubui.


Ndiyo maana hata mawe yatalalamika juu ya ukuta, na miti ya nyumba itayaunga mukono.


Yawe wa majeshi anasema: Kisha nitawakaribia kwa kuwahukumu. Sitasita kutoa ushuhuda juu ya wachawi, wazinzi, watoa ushuhuda wa uongo, wanaopunja mushahara wa watumishi, wanaowatesa wajane na wayatima, wanaozuia mugeni asipate haki yake na wale wasioniogopa mimi.


Halafu akawaambia wanafunzi wake: “Mavuno ni mengi, lakini wavunaji ni wachache.


Basi, Mungu hatawapatia haki wale wachaguliwa wake wanaomulilia usiku na muchana? Au atakawia kuwasaidia?


Ni kama vile Isaya alivyokuwa ametangulia kusema: “Kama Bwana wa Majeshi hangetuponyeshea wamoja wa wazao wetu, ingetutokea sawa Sodoma, ingegeuka kwetu sawa Gomora.”


Muangalie wazo ovu lisiwaingie ndani ya mioyo yenu, mukisema: ‘Mwaka wa saba, mwaka wa kusamehe wadeni uko karibu’. Mukimwangalia ndugu yenu masikini na jicho baya na kukataa kumupa chochote, yeye anaweza kumulilia Yawe juu yenu na hiyo itakuwa zambi kwenu.


Ninyi wabwana muwatendee watumishi wenu kwa usawa na kwa haki, mukijua kwamba ninyi vilevile muko na Bwana wenu katika mbingu.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ