Nitawatafuta kondoo waliopotea na waliotangatanga nitawarudisha kwa nyumba. Waliovunjika nitawatunza, na wale wanaokuwa zaifu nitawapatia nguvu. Lakini kondoo wanono na wenye nguvu nitawaangamiza. Mimi nitawachunga kondoo kama inavyostahili.
Wanaokuwa zaifu hamukuwatia nguvu, wagonjwa hamukuwatunza, waliovunjika hamukuwafunga kwa kitambaa, waliotangatanga hamukuwarudisha na waliopotea hamukuwatafuta. Lakini mukawatawala kwa kinguvu na kuwatesa.
Wandugu zangu, kama mutu akipatikana na kosa fulani, ninyi munaoongozwa na Roho wa Mungu mumwonye mutu yule kwa roho ya upole. Na kila mumoja wenu ajiangalie mwenyewe, kusudi asijaribiwe vilevile.
Kwa maana kupenda feza ni shina la mabaya yote. Kwa ajili ya kuzitamani watu wamoja wanaanguka katika imani yao, na wanajiumiza mioyo wakijiletea huzuni nyingi.
Ole kwao! Maana wamefuata njia ya Kaina. Kwa ajili ya kupata mali wameanguka katika kosa Balama alilofanya. Wameangamia kwa sababu wameasi kama vile Kora alivyoasi.