Yesu akawajibu: “Kwa sababu imani yenu ni ndogo. Kweli ninawaambia kama mukiwa na imani, hata ikiwa tu kama punje ndogo sana ya mbegu ya haradali, mutaweza kuuambia mulima huu: ‘Toka hapa uende kule,’ nao utatoka pale. Hakuna kitu chochote kitakachokosa kuwezekana kwenu. [
Mungu alikusudia kuwaokoa wale wanaomwamini kwa njia ya mahubiri tunayotangaza yanayoonekana kuwa mambo ya upumbafu. Amefanya vile kwa sababu, kwa njia ya hekima yao ya kimutu, watu hawakumutambua Mungu na hekima yake ya kimungu.
Lakini inafaa aombe kwa imani pasipo kuwa na mashaka. Kwa maana mutu anayekuwa na mashaka anafanana na zoruba katika bahari inayosukumwa na upepo na kutupa maji huku na huko.