Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Yakobo 4:3 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

3 Wakati munapoomba, hamupati kitu kwa sababu munaomba kwa nia mbaya, kwa maana munataka vitu kusudi mutimize tu tamaa zenu.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Yakobo 4:3
25 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

naye akamwambia: “Kwa sababu umetoa ombi hili, na haukujiombea maisha marefu au mali, na wala haukuomba waadui zako waangamizwe, lakini umejiombea hekima ya kutoa hukumu au kutenda haki,


Watu wale wanaomba musaada lakini Mungu hawajibu, kwa sababu ya majivuno ya watu waovu.


Uliwakimbiza waadui zangu, na wale walionichukia niliwaangamiza.


Halafu mutaniita lakini sitaitika; mutanitafuta kwa bidii lakini hamutanipata.


Sadaka ya waovu ni chukizo kwa Yawe, lakini maombi ya watu wa usawa yanamufurahisha Mungu.


Anayekataa kusikia kilio cha masikini hatasikilizwa atakapolilia musaada.


Sadaka ya mwovu ni kitu cha kuchukiza sana. Inachukiza zaidi akiitoa kwa nia mbaya.


Kwa hiyo, Yawe anasema hivi: Nitaleta hasara juu yao ambayo hawataweza kuiepuka. Hata kama wakinililia namna gani, sitawasikiliza.


Basi, wewe Yeremia, usiwaombee watu hawa, usinililie kwa ajili yao, wala kunisihi. Maana, hata wakiniomba watakapokuwa katika hasara, sitawasikiliza.


Hata wakifunga, sitayasikiliza maombi yao, na hata wakinitolea sadaka za kuteketeza kwa moto na sadaka zingine, mimi sitazikubali. Lakini nitawaangamiza kwa vita, njaa na ugonjwa mukali.


Wakati unakuja ambapo mutamulilia Yawe, lakini yeye hatawajibu. Atauficha uso wake wakati huo, kwa sababu mumetenda mambo maovu.


nikasema: Kwa sababu niliwaita nao hawakunisikiliza, basi, nao waliponiita, sikuwasikiliza.


Yesu akawaambia: “Hamujui kitu munachoomba. Munaweza kubeba muzigo wa mateso nitakaoubeba?” Nao wakamujibu: “Tunaweza.”


Lakini Yesu akawaambia: “Hamujui kitu munachoomba. Munaweza kunywa kikombe cha mateso nitakachokunywa? Au munaweza kubatizwa kwa namna ya ubatizo nitakaoupata?”


Kwa maana kila mutu anayeomba anapewa; anayetafuta anapata, anayepiga hodi anafunguliwa mulango.


Nyuma ya siku chache, yule mudogo akauzisha urizi wake na kwenda katika inchi ya mbali. Kule aliponda mali yake yote katika maisha ya ovyo.


Lakini mwana wako huyu aliyeharibu mali yako katika ukahaba alipofika, ukamuchinjia yule ngombe mwenye kunona!’


Magombano na ugomvi vinavyokuwa kati yenu vinatoka wapi? Si vinatoka katika tamaa zenu zinazopigana ndani ya miili yenu?


Nasi tunapokea jambo lolote tunaloomba kwake, kwa sababu tunatii amri zake na kutenda mambo yanayomupendeza.


Nasi tuko na tumaini hili mbele ya Mungu: tunajua kwamba atatusikiliza tukimwomba kitu chochote kufuatana na mapenzi yake.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ