Ulijiona salama katika uovu wako; ukajisemesha: Hakuna mutu anayeniona. Hekima na elimu yako vilikupotosha, ukajisemesha ndani ya moyo wako: Mimi ndiye; hakuna mwingine isipokuwa mimi.
Kwa maana kila kitu kinachokuwa katika dunia, kama vile tamaa ya kimwili, tamaa ya macho, na majivuno ya maisha, hivi vyote havitoki kwa Baba, lakini vinatoka katika dunia.
Na kwa kadiri ulivyojitukuza na kuishi katika raha, kwa kadiri ile ile muuletee mateso na huzuni. Muji ule unajisemesha: ‘Mimi ninaikaa juu ya kiti cha kifalme kama vile malkia; mimi si mujane, wala sitapata huzuni hata kidogo!’