15 Ninyi mungepaswa kusema: “Kama Bwana anataka, tutaishi na kufanya hivi na hivi.”
Katika moyo wa mutu muna mipango mingi, lakini anachokusudia Yawe ndicho kitakachokamilika.
Nani anayeweza kusema kusudi kitu kifanyike ikiwa Yawe asipoamuru ikuwe hivyo?
Alipoagana nao, akawaambia: “Kama Mungu akitaka nitarudi huku kwenu tena.” Halafu akaondoka Efeso, akisafiri kwa njia ya chombo.
katika maombi yangu. Ninaomba kwamba Mungu akitaka, anifungulie njia ya kuwatembelea siku hizi.
Na hivi Mungu akitaka, nitakuja kwenu kwa furaha, nami nitapata kutulizwa moyo kati yenu.
Kwa maana sitaki kuonana nanyi kwa kupita tu. Ninatumaini kukaa pamoja nanyi siku chache Bwana akitaka.
Lakini nitakuja kwenu upesi Bwana akitaka. Basi pale nitajua maneno ya wale wanaojivuna na kujionea uwezo wao vilevile!
Lakini sasa munajivuna na kujisifu. Majivuno yote ya namna hii ni mabaya.