14 Ninyi hamujui namna gani maisha yenu yatakavyokuwa kesho! Kwa maana ninyi ni kama muvuke unaoonekana kwa wakati kidogo, kisha unatoweka.
Basi, mufalme Daudi akamwambia Barzilayi: “Twende wote kule Yerusalema nami nitakutunza.”
Usijifiche mbali nami wakati wa taabu! Unitegee sikio lako, unijibu upesi wakati ninapokuomba!
Mwanadamu ni kama pumzi tu; siku zake zinapita kama kivuli.
“Ee Yawe, unijulishe mwisho wangu, siku zangu za kuishi zimenibakia ngapi, nijue namna maisha yangu yanavyopita upesi!”
Alikumbuka kwamba wao ni watu tu; ni kama upepo unaopita na kutoweka.
Ee Yawe, utajificha hata milele? Mpaka wakati gani hasira yako itawaka kama moto?
Usijisifie kwa ajili ya kesho. Haujui siku ya leo itakuletea nini.
Usimutumainie mwanadamu, uzima wake ni kama pumzi tu. Yeye anafaa kitu gani?
Makao yangu yameongolewa kwangu; kama hema la muchungaji; kama, mufumaji nimefika kwa mwisho wa kizingo cha maisha yangu; Mungu amekata nyuzi zinazokishika; hata mbele ya mwisho wa siku amenikomesha.
na ndugu anayekuwa tajiri afurahi kwa sababu Mungu anamushusha. Maana tajiri atatoweka kama maua ya pori.
Kwa maana Maandiko Matakatifu yanasema: “Wanadamu wote ni kama majani. Na utukufu wao wote unatoweka kama maua. Majani yanakauka na maua yanaanguka.
Mwisho wa vitu vyote unakaribia kutimia. Kwa hiyo mukuwe wenye akili na waangalifu, kusudi mukuwe na uwezo wa kuomba.
Dunia inapita pamoja na tamaa zake, lakini mutu yule anayefanya mapenzi ya Mungu anaishi milele.