Mara nyingi miguu yake ilifungwa vifungo vya chuma, nayo mikono yake na minyororo, lakini alikata minyororo ile na kuvunjavunja vile vifungo vya chuma. Hakuna mutu aliyekuwa na nguvu ya kumushinda.
Nao ulimi ni kama moto. Ulimi ni kiungo kinachojaa ubaya wa kila namna. Ulimi unapatikana kwenye nafasi yake katikati ya viungo vyetu, nao ndio unaochafua mwili wote. Unateketeza maisha yetu ukichomwa wenyewe na moto unaotoka katika jehenamu.