Lakini Onani alijua kwamba hao watoto hawangekuwa wake. Kwa hiyo, alipolala na muke wa ndugu yake, alimwanga chini mbegu ya uzazi, kusudi asimupatie ndugu yake watoto.
Lakini Yehu hakutii sheria za Yawe, Mungu wa Israeli, kwa moyo wake wote. Hakuacha zambi zile za Yeroboamu ambaye aliwasukuma watu wa Israeli watende zambi.
kwa sababu mungali munatawaliwa na mambo ya kidunia. Kwa maana ikiwa kungali wivu na ugomvi katikati yenu, haionyeshi kwamba munatawaliwa na mambo ya kidunia, nanyi munaishi kufuatana na hali ya kimutu?
Kwa maana ninaogopa kwamba wakati ninapokuja kwenu, sitawakuta sawa vile ninavyotaka, nanyi hamutanikuta sawa vile munavyotaka. Ninaogopa kuwakuta katika fitina, wivu, kasirani, ugomvi, masingiziano, matetano, majivuno na fujo.
chuki, uuaji, ulevi, ulafi, na mambo mengine yanayofanana na hayo. Ninawaonya tena kama vile nilivyowaonya mbele, kwamba watu wanaotenda mambo kama hayo hawatashiriki katika Ufalme wa Mungu.
Watu hao wanaotahiriwa, hawashiki Sheria lakini wanataka mutahiriwe kusudi wapate kujivuna kwamba wanawashurutisha kuwa na kitambulisho kile juu ya mwili wenu.
Musifanye jambo lolote kwa roho ya mapingano wala kwa kujivuna bure, lakini munyenyekeane kila mutu akimuhesabu mwenzake kuwa muzuri kuliko yeye mwenyewe.
yeye anajaa majivuno wala hajui kitu. Yeye yuko na ulema wa kubishana na kugombezana juu ya maana ya maneno. Na hayo yanaleta wivu, makelele, matukano, masingiziano
Kwa maana zamani sisi vilevile tulikuwa wajinga, waasi na wapotovu. Tulikuwa tumetawaliwa na kila namna ya tamaa mbaya na ya vitu mbalimbali vilivyotuvuta sana. Tuliishi katika uovu na wivu, tuliwachukiza watu nao walituchukia.