Wakati waliposikia maneno haya, wakaondoka wote mumoja kwa mumoja, wakianzia kwa wazee. Yesu akabaki pale peke yake pamoja na yule mwanamuke aliyekuwa akisimama mbele yake.
Kwa sababu hakuna mutu atakayehesabiwa haki mbele ya Mungu kwa kuwa anatii Sheria, maana Sheria inamusaidia mutu tu kwa kutambua kwamba amefanya zambi.
Lakini kama wote wakitabiri, na kama mutu mumoja asiyeamini au asiyeelewa kitu anaingia, atapata uhakikisho kutokana na maneno ya hao wote. Naye atahukumiwa kufuatana na yote aliyosikia na
Maana kufuatana na Sheria hiyo, mimi nimekuwa kama mufu, na kifo kile kimesababishwa na Sheria. Imetokea vile kusudi nipate kuishi kwa ajili ya Mungu. Mimi nimekufa pamoja na Kristo juu ya musalaba.
Musipendelee mutu yeyote katika kutoa hukumu; mutawasikiliza bila upendeleo, wakubwa kwa wadogo. Musiogopeshwe na sura ya mutu, maana ninyi mutapaswa kuhukumu kwa ajili ya Mungu. Kukikuwa maneno ambayo ni magumu sana kwenu, mutayafikisha kwangu nami nitayasikiliza.’
Atakuja kuwahukumu wote na kuwaazibu watu wabaya wasiomwogopa Mungu, kwa ajili ya matendo yao yote mabaya waliyotenda, na kwa ajili ya maneno yote mabaya wenye zambi hawa waliyosema juu yake.”