Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Yakobo 2:8 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

8 Munafanya vizuri kama mukitimiza sheria hii ya kifalme inayopatikana katika Maandiko Matakatifu: “Umupende mwenzako kama unavyojipenda wewe mwenyewe.”

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Yakobo 2:8
23 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Lakini Yawe alimwambia baba yangu Daudi: ‘Ni vizuri kwamba ulikusudia ndani ya moyo wako kunijengea nyumba.


Lakini wakaambiana: “Tunalofanya si sawa! Hii ni habari njema tunayokuwa nayo leo, na ikiwa tutangoja mpaka asubui, bila shaka tutaazibiwa. Tuende mara moja tuwaambie watu wa nyumba ya mufalme!”


Usijilipize kisasi au kuwa na kinyongo juu ya wazao wa watu wako lakini umupende mwenzako kama vile unavyojipenda wewe mwenyewe. Mimi ni Yawe.


Huyo mugeni anayekaa nawe atakuwa kwako kama vile mwenyeji nawe utamupenda kama vile unavyojipenda mwenyewe, kwa sababu nawe ulikuwa mugeni katika inchi ya Misri. Mimi ni Yawe, Mungu wenu.


Naye Yawe akamujibu Yona: Unazani kwamba unafanya vema kukasirika?


Lakini Mungu akamwuliza Yona: Unazani unafanya vema kuukasirikia mumea huo? Yona akajibu: Ndiyo, ninafanya vema kukasirika – kukasirika hata kufa!


Na ya pili inayofanana nayo ni hii: ‘Umupende mwenzako kama vile unavyojipenda mwenyewe.’


Bwana wake akamwambia: ‘Ni vizuri, wewe mutumishi mwema na mwaminifu. Ulikuwa mwaminifu katika ulinzi wa mali ndogo, basi nitakuweka kuwa mulinzi wa mali mengi. Kuja ufurahi pamoja na bwana wako.’


Bwana wake akamwambia: ‘Ni vizuri, wewe mutumishi mwema na mwaminifu. Ulikuwa mwaminifu katika ulinzi wa mali ndogo, basi nitakuweka kuwa mulinzi wa mali mingi. Kuja ufurahi pamoja na bwana wako!’


“Basi jambo lolote munalotaka wengine wawatendee, ninyi mulitende kwao vilevile, kwa maana kile ndicho kifungo cha Sheria ya Musa na mafundisho ya manabii.


Anayemupenda mwenzake hawezi kumutendea vibaya. Basi Sheria inatimizwa kwa njia ya upendo.


Kwa maana Sheria yote inafungwa katika amri hii moja: “Umupende mwenzako kama unavyojipenda mwenyewe.”


Musaidiane ninyi kubeba mizigo yenu, na hivi mutatimiza sheria ya Kristo.


Lakini, mumefanya vizuri kwa kushirikiana pamoja nami katika taabu yangu.


Na kuelekea upendo wa wandugu waamini, si lazima kwenu kuwaandikia neno lolote, kwa maana Mungu yeye mwenyewe amewafundisha ninyi kupendana.


Lakini mutu anayechunguza sheria kamilifu inayoweka watu huru na kuendelea kushikamana nayo, na si kuisikia tu na kisha kuisahau, lakini anaitimiza kabisa, mutu huyu atabarikiwa na Mungu katika shuguli zake.


Basi museme na kutenda kama watu watakaohukumiwa kufuatana na sheria inayotuweka kuwa huru.


Si wewe unaamini kwamba kuna Mungu mumoja? Ni vizuri! Hata pepo wanaamini vile, nao wanatetemeka kwa woga.


Wandugu, musisemeane ubaya. Yule anayesema ubaya juu ya ndugu yake au kumuhukumu, anasema ubaya juu ya Sheria na kuihukumu. Ukihukumu Sheria, wewe si mwenye kutii Sheria, lakini mwenye kuihukumu.


Lakini ninyi ni watu wa kizazi kilichochaguliwa na Mungu na wa ukuhani wa kifalme. Ninyi ni taifa takatifu na watu wa pekee wa Mungu. Mumechaguliwa kusudi mutangaze matendo makubwa ya yule aliyewaita kutoka katika giza na kuwaingiza kwenye mwangaza wake wa ajabu.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ