26 Kwa maana kama vile mwili usiokuwa na pumzi ndani yake umekufa, hivi vilevile imani pasipo matendo imekufa.
Ukiwageuzia mugongo, wanaogopa; ukiondoa pumzi yao, wanakufa na kurudi ndani ya mavumbi walimotoka.
Mwanadamu akitoa pumzi yake ya mwisho, anarudi katika mavumbi alimotoka, na hapo mipango yake yote inatoweka.
mavumbi yanarudilia inchi tena, na roho inamurudilia Mungu aliyeipana.
Usimutumainie mwanadamu, uzima wake ni kama pumzi tu. Yeye anafaa kitu gani?
Yesu akalalamika kwa sauti kubwa akisema: “Baba, ninatoa uzima wangu kwako.” Kisha kusema maneno haya, akakata roho.
Kwa maana kwa wale wanaoungana na Kristo Yesu, kutahiriwa au kutokutahiriwa hakufai kitu. Kitu kinachofaa ni imani inayotenda kazi kwa upendo.
Wandugu zangu, ni faida gani kama mutu akisema kwamba yuko na imani lakini haionyeshi kwa njia ya matendo mazuri? Ile imani itaweza kumwokoa?
Ni hivi vilevile, imani peke yake pasipo matendo imekufa kabisa.
Wewe mujinga! Unataka kuhakikishwa kwamba imani pasipo matendo ni bure?