24 Basi munaona kwamba mutu anahesabiwa haki mbele ya Mungu kwa njia ya matendo, wala si kwa njia ya imani peke yake.
Si wewe Mungu ambaye umetutupilia? Lakini hauendi tena na jeshi letu.
Kwa maana tunaona kama mutu anahesabiwa haki mbele ya Mungu kwa njia ya imani wala si kwa njia ya kutii Sheria.
Na maandiko haya yakatimia: “Abrahamu alimwamini Mungu na kwa hiyo akahesabiwa kuwa mwenye haki.” Na Mungu akamwita rafiki yake.
Ilikuwa hivi vilevile kwa yule kahaba Rahaba. Mungu alimuhesabia haki kwa njia ya matendo yake, wakati alipowakaribisha wapelelezi na kuwatorosha kwa njia nyingine.