Si wewe, ee Mungu wetu, uliyewafukuza wenyeji wa inchi hii wakati watu wako Waisraeli walipoingia katika inchi hii, ukawapa wazao wa Abrahamu rafiki yako, ikuwe yao milele?
Hivi ndivyo Yawe alivyokuwa akiongea na Musa uso kwa uso, kama mutu na rafiki yake. Kisha Musa alirudi tena katika kambi. Naye kijana Yoshua mwana wa Nuni ambaye alikuwa mutumishi wake hakuondoka ndani ya hema.
“Wandugu zangu, ilikuwa lazima yale Maandiko Matakatifu yatimie ambayo Roho Mutakatifu alitabiri kwa kinywa cha mufalme Daudi juu ya Yuda, yule aliyewaongoza wale waliomukamata Yesu.
Mungu hakuwakataa watu wake aliojichagulia tangu mbele. Munakumbuka Maandiko Matakatifu yanayosema juu ya mashitaki ya Elia mbele ya Mungu juu ya Waisraeli? Yeye alisema:
Mungu anamwambia mufalme wa Misri katika Maandiko Matakatifu: “Nimekusimika kuwa mufalme kwa sababu hii moja, ni kusudi kwa njia yako nipate kuonyesha uwezo wangu na kusudi jina langu lipate kutangazwa katika dunia yote.”
Lakini Maandiko Matakatifu yanasema kwamba watu wote wako chini ya utumwa wa zambi, kusudi zawadi iliyoahidiwa na Mungu itolewe kwa wale wanaoamini kwa njia ya imani yao katika Yesu Kristo.
Kwa kuwa imeandikwa hivi katika Maandiko Matakatifu: “Nimesimika jiwe kubwa la pembe katika Sayuni, jiwe lile ni la bei kali. Ni mimi niliyelichagua. Yule anayelitumainia hatapata haya.”