Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Yakobo 2:18 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

18 Lakini mutu anaweza kusema: “Wewe uko na imani, na mimi niko na matendo.” Mimi nitajibu: “Unionyeshe imani yako pasipo matendo, na mimi nitakuonyesha imani yangu kwa njia ya matendo yangu.”

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Yakobo 2:18
20 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Lakini mutu anayekuwa na mashaka juu ya chakula anachokula, Mungu anamuhukumu, kwa sababu hatendi kufuatana na imani. Na kitendo chochote kisichotokana na imani ni zambi.


Kwa maana tunaona kama mutu anahesabiwa haki mbele ya Mungu kwa njia ya imani wala si kwa njia ya kutii Sheria.


Na ni vile Daudi anavyosema juu ya uheri wa mutu ambaye Mungu anayehesabia haki pasipo kuangalia matendo yake.


Basi sasa hakuna azabu kwa wale wanaoungana na Yesu Kristo.


Labda utaniambia: “Ikiwa ni vile, sababu gani Mungu anawashitaki watu? Kwa maana hakuna anayeweza kupingana na mapenzi yake.”


Hata nikiwa na zawadi ya kutabiri, na uwezo wa kujua mafumbo yote na maarifa yote; hata nikiwa na imani kubwa inayoweza kuhamisha milima; lakini kama sina upendo, mimi ni kitu bure.


Basi mutu yeyote anapoungana na Kristo, yeye anakuwa kiumbe kipya. Mambo ya zamani yametoweka, na sasa hali mupya imefika.


Basi wapendwa wangu, kwa kuwa tumepewa ahadi hizi zote, tujitakase toka uchafu wote unaochafua mwili na roho na tujikaze kuwa watakatifu kabisa tukiishi katika kumuheshimu Mungu.


Kwa maana kwa wale wanaoungana na Kristo Yesu, kutahiriwa au kutokutahiriwa hakufai kitu. Kitu kinachofaa ni imani inayotenda kazi kwa upendo.


Shabaha ya agizo hilo ni kusudi kuwe upendo unaotokana na moyo safi na zamiri nzuri na imani ya kweli.


Na wewe unapaswa kuwa mufano katika matendo mema, ukionyesha ukweli na heshima katika mafundisho yako.


Kwa njia ya imani, Rahaba, yule kahaba, hakuangamia pamoja na wale waliomwasi Mungu, kwa sababu aliwakaribisha wapelelezi kwa amani.


Kwa njia ya imani hawa walishinda inchi za wafalme, walitenda mambo ya haki na kupata yale Mungu aliyowaahidi. Walifunga vinywa vya simba,


Basi pasipo imani, hakuna mutu anayeweza kumupendeza Mungu. Kwa maana mutu anayetaka kumwendea Mungu sherti aamini kwamba Mungu yuko, na kwamba anawapa zawadi wale wanaomutafuta.


Wandugu zangu, ni faida gani kama mutu akisema kwamba yuko na imani lakini haionyeshi kwa njia ya matendo mazuri? Ile imani itaweza kumwokoa?


Nani anayekuwa na hekima na ufahamu kati yenu? Basi aonyeshe jambo lile kwa njia ya mwenendo wake muzuri, kwa njia ya matendo yanayofanyika katika upole unaotokana na hekima ile.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ