Kisha wakasemezana wao kwa wao: “Kweli sisi tulimukosea ndugu yetu. Ingawa tulimwona katika taabu, hatukumujali hata alipotusihi. Ndiyo maana taabu hii yote inatupata.”
Matawi ya miti yamekauka na kuvunjika; wanawake wanayaokota na kuyawasha moto. Watu hawa hawajaelewa kitu, kwa hiyo Mungu, Muumba wao, hatawahurumia, yeye aliyewafanya, hatawatendea mema.
Basi, uwaambie: Kama vile ninavyoishi, –ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe– mimi sikifurahii kifo cha mutu mwovu, lakini ninapenda mutu mwovu aachane na mwenendo wake mubaya, apate kuishi. Mugeuke, muachane na mwenendo wenu mubaya, enyi Waisraeli! Kwa nini munataka kufa?
Ee Mungu, ni nani anayekuwa kama wewe? Wewe unasemehe zambi za watu wako waliobaki, wala hauyaangalii makosa yao. Hasira yako haidumu milele, lakini unapendelea zaidi kutuonyesha wema wako.
Lakini Abrahamu akamujibu: ‘Mutoto wangu, kumbuka kwamba umekwisha kupewa mema yaliyokupasa wakati ulipoishi katika dunia, na Lazaro alipata taabu. Na sasa yeye anatulizwa, lakini wewe unateswa.
“Musiwahukumu wengine, na Mungu hatawahukumu ninyi. Musikuwe wenye kukatia wengine azabu, naye hatawaazibu ninyi. Muwasamehe wengine, na Mungu atawasamehe ninyi vilevile.
Lakini hekima inayotoka mbinguni, kwanza ni safi, tena ni yenye amani, upole na usikilivu, inajaa huruma na matendo mema. Haina upendeleo wala udanganyifu.
Ninyi hamukulipa mishahara ya watumishi waliotumika katika mashamba yenu. Musikilize mashitaki yao! Malalamiko ya wavunaji yamefika katika masikio ya Bwana Mwenye Uwezo!
Adoni-Bezeki akasema: “Wafalme makumi saba waliokatwa vidole gumba vya mikono na miguu waliokota makombo chini ya meza yangu. Sasa Mungu amenilipa kama nilivyotenda.” Wakamupeleka Yerusalema, akakufia kule.