Nao walifika, wakaitwaa na kuirizi. Lakini wao hawakukusikiliza, wala hawakufuata sheria zako. Hawakutenda mambo uliyoamuru. Ndiyo maana utawafanya wapatwe na hasara hii.
Lakini wale wanaotegemea kutimiza yale yanayoamuriwa na Sheria, wamelaaniwa. Kwa maana Maandiko Matakatifu yanasema: “Alaaniwe mutu yeyote asiyedumu katika yote yanayoandikwa katika hiki kitabu cha Sheria na kuyatii.”
Kwa hiyo wandugu zangu, kufuatana na vile mulivyochaguliwa na kuitwa na Mungu, mufanye nguvu zaidi kwa kukamilika katika njia ile. Mukitenda mambo yale hamutaanguka hata kidogo.