Yakobo 1:27 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
27 Dini inayokuwa safi na bila kosa mbele ya Mungu Baba ndiyo hii: kushugulikia wayatima na wajane wanaoteswa, na kujilinda mwenyewe na uchafu wa dunia hii.
Wakubwa wako ni waasi; wanashirikiana na wizi. Kila mumoja anapenda kituliro, na kukimbilia zawadi. Hawamupatii yatima haki yake, haki za wajane si kitu kwao.
Kila mutu anayesema vibaya juu ya Mwana wa Mutu atasamehewa, lakini kila mutu anayesema vibaya juu ya Roho Mutakatifu, hatasamehewa katika ulimwengu huu, wala katika ule unaokuja.
Musifuate mwenendo wa siku hizi, lakini muache Mungu awabadilishe kwa kugeuza upya nia zenu, hata mukuwe na mawazo mapya. Kwa hiyo mutaweza kutambua mapenzi ya Mungu. Mutajua mambo gani yanayokuwa mema, yanayomupendeza Mungu na yanayokuwa makamilifu.
Na zaidi ya hii ni wazi kwamba hakuna mutu anayehesabiwa haki mbele ya Mungu kwa njia ya Sheria. Kwa maana Maandiko Matakatifu yanasema: “Mwenye haki ataishi kwa njia ya imani.”
Na mimi kwa ngambo yangu sitaki kujivuna, isipokuwa tu kwa ajili ya musalaba wa Bwana wetu Yesu Kristo. Maana kwa njia ya musalaba huo, ninahesabu dunia kama vile imekwisha kufa na mbele ya dunia mimi ninahesabiwa kama vile mufu.
Hiyo itakuwa kwa ajili ya Walawi, kwa sababu hawana fungu wala urizi wao kati yenu, nao wageni, wayatima na wajane ambao wanaishi katika miji yenu, watakuja kula na kushiba. Mufanye hivi naye Yawe, Mungu wenu, atawabariki katika kazi zenu zote munazofanya kwa mikono yenu.
Lakini kama mujane akiwa na watoto au wajukuu, inafaa wajifunze kwanza kutimiza mapaswa yao ya kidini kwa ajili ya jamaa zao wenyewe na kuwarudishia wazazi na babu zao mema waliyowatendea, kwa maana jambo hilo linamupendeza Mungu.
Neema hii inatufundisha kwamba tuache uovu na tamaa za dunia, na kuishi katika dunia hii ya sasa katika ukadirifu, katika haki na kushikamana na ibada.
Lakini hekima inayotoka mbinguni, kwanza ni safi, tena ni yenye amani, upole na usikilivu, inajaa huruma na matendo mema. Haina upendeleo wala udanganyifu.
Ninyi watu wasiokuwa na uaminifu! Hamujui kwamba kupenda raha ya dunia ni kuwa adui wa Mungu? Basi yeye anayetaka kupenda raha za dunia anajifanya mwenyewe kuwa adui wa Mungu.
Kufuatana na hayo, ikiwa watu wamekwisha kuponyoka kuishi katika machafuko ya dunia kwa njia ya kumujua Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo, nao wakiyarudilia tena na kutawaliwa nayo, hali yao ya mwisho itakuwa mbaya zaidi kuliko ile ya kwanza!