Kila siku, tangu siku ya kwanza mpaka ya mwisho, Ezra aliwasomea watu kitabu cha Sheria ya Mungu. Wakafanya sikukuu ile kwa muda wa siku saba. Na siku ya nane wakafanya mukutano mukubwa wa kufunga sikukuu, kama vile ilivyoagizwa.
Wakakataa kutii; hawakukumbuka maajabu uliyofanya kati yao. Wakakuwa wagumu, wakajichagulia kiongozi wa kuwarudisha katika utumwa katika inchi ya Misri. Lakini wewe Mungu uko mwepesi kwa kusamehe, mwenye huruma na rehema, haukasiriki upesi, uko mwema sana. Haukuwatupilia
Kwa muda wa yapata saa tatu, walisimama wakati Sheria ya Yawe, Mungu wao, ikisomwa. Na kwa saa tatu zilizofuata, walikuwa wakitubu na kumwabudu Yawe, Mungu wao.
Na pale pale nikatuma watu kwako, nawe umefanya vizuri kwa kufika. Sasa sisi wote tuko hapa mbele ya Mungu kwa kusikiliza mambo yote Bwana aliyokuagiza kutuambia.”
Wakati watu wa mataifa mengine waliposikia maneno haya wakafurahi, wakatukuza neno la Bwana. Nao wote waliokuwa wamechaguliwa kwa kupata uzima wa milele, wakaamini.
Watu hao walikuwa wenye nia nzuri zaidi kuliko watu wa Tesalonika; nao walipokea Neno la Mungu kwa hamu kubwa. Kila siku walichunguza Maandiko Matakatifu wapate kujua kwamba maneno Paulo aliyosema yalikuwa ya haki.
Inatupasa tena kumushukuru Mungu siku zote kwa ajili ya jambo hili: muliposikia neno la Mungu kutoka kwetu, hamukulikubali kama vile neno la mutu, lakini kama vile kweli ndilo neno la Mungu. Na neno lile ndilo linalofanya kazi ndani ya mioyo yenu ninyi wanaoamini.
Wandugu zangu wapenzi, musikilize: Mungu amewachagua wamasikini wa dunia hii kusudi wakuwe watajiri katika imani, nao wapokee Ufalme ule aliowaahidi wale wanaomupenda.
Wandugu, musisemeane ubaya. Yule anayesema ubaya juu ya ndugu yake au kumuhukumu, anasema ubaya juu ya Sheria na kuihukumu. Ukihukumu Sheria, wewe si mwenye kutii Sheria, lakini mwenye kuihukumu.
Lakini zaidi ya yote, wandugu zangu, musiape! Musiape kwa jina la mbingu, wala kwa jina la dunia, wala kwa jina la kitu kingine chochote. Museme “Ndiyo” ikiwa munataka kusema ndiyo. Nanyi museme “Hapana” ikiwa munataka kusema hapana, kusudi musihukumiwe na Mungu.