Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Yakobo 1:19 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

19 Wandugu zangu wapendwa, mukumbuke neno hili: kila mutu anapaswa kuwa mwepesi kwa kusikia, lakini asikuwe mwepesi kwa kusema na kukasirika.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Yakobo 1:19
54 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Kila siku, tangu siku ya kwanza mpaka ya mwisho, Ezra aliwasomea watu kitabu cha Sheria ya Mungu. Wakafanya sikukuu ile kwa muda wa siku saba. Na siku ya nane wakafanya mukutano mukubwa wa kufunga sikukuu, kama vile ilivyoagizwa.


Wakakataa kutii; hawakukumbuka maajabu uliyofanya kati yao. Wakakuwa wagumu, wakajichagulia kiongozi wa kuwarudisha katika utumwa katika inchi ya Misri. Lakini wewe Mungu uko mwepesi kwa kusamehe, mwenye huruma na rehema, haukasiriki upesi, uko mwema sana. Haukuwatupilia


Kwa muda wa yapata saa tatu, walisimama wakati Sheria ya Yawe, Mungu wao, ikisomwa. Na kwa saa tatu zilizofuata, walikuwa wakitubu na kumwabudu Yawe, Mungu wao.


Basi, ningoje tu kwa vile hamusemi, kwa sababu munakaa tu bila kujibu kitu?


Kwenye kuwa maneno mengi hakukosekani makosa, lakini aneyezuia ulimi wake ana akili.


Anayechunga kinywa chake analinda maisha yake, mwenye midomo mirefu anajiletea maangamizi.


Mwenye kuwaka hasira haraka anatenda kipumbafu, lakini mwenye akili ana uvumilivu.


Mutu asiyekuwa mwepesi wa hasira ana akili nyingi, lakini anayekasirika upesi anaongeza upumbafu.


Mutu wa hasira mbaya anasababisha ugomvi, lakini asiyekuwa mwepesi wa hasira anautuliza.


Ulimi wa mwenye hekima unaeneza maarifa, lakini watu wapumbafu wanamwanga maneno ya ujinga.


Asiyekuwa mwepesi wa hasira ni bora kuliko mwenye nguvu. Anayetawala nafsi yake ni bora kuliko anayetaka muji.


Kuanzisha ugomvi ni kama kufungua maji ya kisima; achana na ugomvi mbele haujafurika.


Asiyesema sana ana maarifa; mutu mutulivu ni mwenye ufahamu.


Kujibu mbele ya kusikiliza ni upumbafu na jambo la haya.


Ulimi una nguvu ya kuleta uzima na kuua; wanaopenda kuutumia watakula matunda yake.


Mwenye akili hakasiriki upesi; kusamehe makosa ni utukufu kwake.


Mutu wa hasira kali anapaswa kupata azabu; ukimwachilia mara moja itakuomba kumwachilia tena.


Anayechunga kinywa chake na ulimi wake, anajiepusha na matatizo.


Mutu asiyeweza kuzuia hasira yake ni kama muji usiokuwa na ulinzi unaposhambuliwa.


Unamwona mutu anayesema bila kufikiri? Mutu mupumbafu ni afazali kuliko yeye.


Punda alipomwona huyo malaika wa Yawe, akalala chini. Balamu akawaka hasira, akamupiga kwa fimbo yake.


Lakini mimi ninawaambia: mutu yeyote anayemukasirikia ndugu yake anapaswa kuhukumiwa. Naye anayemwambia ndugu yake: ‘Hauna akili wewe!’ anapaswa kupelekwa kwenye tribinali kubwa. Naye anayemwambia: ‘Uko mwenda-wazimu!’ anastahili kutupwa katika jehenamu.


Daudi mwenyewe anamwita Kristo ‘Bwana’; namna gani basi Kristo anaweza kuwa Mwana wake?” Kundi kubwa la watu walimusikiliza Yesu kwa furaha.


Watu wengi wakakusanyika pale mpaka hapakukuwa tena nafasi ndani ya nyumba, hata inje mbele ya mulango. Yesu alipokuwa akiwahubiri Neno la Mungu,


Siku moja walipishaji wa kodi na watenda mabaya wengi walikusanyika karibu na Yesu kwa kumusikiliza.


Lakini hawakupata namna ya kumwua, kwa sababu watu wote walimusikiliza kwa uangalifu.


Katika siku zile, kulikuwa mukutano wa wandugu waamini yapata watu mia moja makumi mbili. Basi Petro akasimama katikati yao, akasema:


Na pale pale nikatuma watu kwako, nawe umefanya vizuri kwa kufika. Sasa sisi wote tuko hapa mbele ya Mungu kwa kusikiliza mambo yote Bwana aliyokuagiza kutuambia.”


Wakati watu wa mataifa mengine waliposikia maneno haya wakafurahi, wakatukuza neno la Bwana. Nao wote waliokuwa wamechaguliwa kwa kupata uzima wa milele, wakaamini.


Watu hao walikuwa wenye nia nzuri zaidi kuliko watu wa Tesalonika; nao walipokea Neno la Mungu kwa hamu kubwa. Kila siku walichunguza Maandiko Matakatifu wapate kujua kwamba maneno Paulo aliyosema yalikuwa ya haki.


Nao walikuwa wakijitoa kufuata mafundisho ya mitume, kuishi katika ushirika wa kindugu, kumega mukate na kuomba.


Kama mukikasirika, musianguke katika zambi, kasirani yenu isidumu muchana kutwa,


Mutupilie mbali nanyi nia zote za uadui, chuki, kasirani, fujo na masingizio. Mutupilie mbali ubaya wa kila namna!


Amani ya Kristo itawale katika mioyo yenu; maana ni kwa ajili ya hiyo ninyi mumeitwa kuwa katika mwili mumoja. Mukuwe wenye shukrani.


Lakini sasa mutupilie mbali mambo haya yote: kasirani, chuki, uovu, masingiziano na musiseme neno lolote baya.


Inatupasa tena kumushukuru Mungu siku zote kwa ajili ya jambo hili: muliposikia neno la Mungu kutoka kwetu, hamukulikubali kama vile neno la mutu, lakini kama vile kweli ndilo neno la Mungu. Na neno lile ndilo linalofanya kazi ndani ya mioyo yenu ninyi wanaoamini.


Wandugu zangu, muhesabu kuwa ni jambo la furaha sana wakati munapopata majaribu ya namna mbalimbali,


Kama mutu akizani kwamba yeye ni mutu wa dini naye hawezi kuzuiza ulimi wake, anajidanganya mwenyewe, nayo dini yake haina faida.


Wandugu zangu, kufuatana na vile munavyomwamini Bwana wetu Yesu Kristo mwenye utukufu, musikuwe vilevile na upendeleo na watu.


Wandugu zangu wapenzi, musikilize: Mungu amewachagua wamasikini wa dunia hii kusudi wakuwe watajiri katika imani, nao wapokee Ufalme ule aliowaahidi wale wanaomupenda.


Ndani ya kinywa kimoja munatoka maneno ya sifa na ya laana. Wandugu zangu, mambo haya hayapaswi kuwa vile.


Wandugu, musisemeane ubaya. Yule anayesema ubaya juu ya ndugu yake au kumuhukumu, anasema ubaya juu ya Sheria na kuihukumu. Ukihukumu Sheria, wewe si mwenye kutii Sheria, lakini mwenye kuihukumu.


Lakini zaidi ya yote, wandugu zangu, musiape! Musiape kwa jina la mbingu, wala kwa jina la dunia, wala kwa jina la kitu kingine chochote. Museme “Ndiyo” ikiwa munataka kusema ndiyo. Nanyi museme “Hapana” ikiwa munataka kusema hapana, kusudi musihukumiwe na Mungu.


Wandugu zangu, mutu mumoja kati yenu akipotea mbali na ukweli, na mutu mwingine akimurudisha,


Basi, sikuwaandikia kwa sababu hamujui ukweli, lakini kwa sababu munaujua na tena kwa sababu hakuna uongo wowote unaoweza kutokana na ukweli.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ