Yakobo 1:11 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
11 Jua linatokea na kwa joto kali linakausha mimea, nayo maua yake yanaanguka na uzuri wake wote unaharibika. Hivi ndivyo tajiri naye atakavyotoweka katika shuguli zake.
Ole wa Samaria, muji unaokuwa kama taji juu ya bonde kwenye udongo muzuri. Walevi wa ajabu wa Efuraimu wanajivuna kwa ajili yake, lakini utukufu wake utatoweka kama ua linalonyauka!
utukufu wake unatoweka kama ua linalonyauka; utukufu uliotawala katika bonde kwenye udongo muzuri utakuwa kama tini za mwanzo mbele ya wakati wa mavuno; mutu akiziona anazichuma na kuzikula mara moja.
Hawatasikia tena njaa wala kuwa na kiu. Upepo wenye kuunguza wala jua havitawachoma, mimi niliyewahurumia nitawaongoza na kuwapeleka kwenye chemichemi za maji.
Wakasema: ‘Watumishi hawa wa mwisho wametumika kazi kwa saa moja tu, nawe umewalipa sawasawa na sisi tuliovumilia muchoko na jua kali kwa muchana kutwa!’
Basi ikiwa Mungu anavalisha majani kama hivi, yanayoonekana leo na kesho yanatoweka na kutupwa katika moto, hatawavalisha ninyi vizuri zaidi, ninyi wenye imani ndogo?
na hivyo tutapata baraka zile ambazo Mungu aliwawekea watu wake. Baraka zisizoweza kuoza wala kuchafuka wala kupunguka; nazo zinawekewa akiba kwa ajili yenu mbinguni.