Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Yakobo 1:1 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

1 Barua hii inatoka kwangu mimi Yakobo, mutumishi wa Mungu na wa Bwana Yesu Kristo. Ninawasalimia ninyi watu wa makabila kumi na mawili waliosambazwa katika dunia.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Yakobo 1:1
41 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Alitwaa mawe kumi na mawili, hesabu ya makabila kumi na mawili yaliyopewa majina ya wana wa Yakobo ambaye neno la Yawe lilimufikia kusema hivi: “Jina lako litakuwa Israeli.”


Wakati wa kuizindua nyumba ya Mungu, walitoa ngombe dume mia moja, kondoo dume mia mbili, wana-kondoo mia ine na beberu kumi na wawili kwa ajili ya sadaka ya kusamehewa zambi, mbuzi mumoja kwa kila kabila la Israeli.


Basi, Hamani akamwambia mufalme: “Kuna watu wa taifa moja wanaokuwa kila nafasi katika utawala wako, nao wako katika kila jimbo. Watu hao wana sheria zinazokuwa tofauti kabisa na za watu wengine. Vilevile, wao hawazitii sheria zako, kwa hiyo haikufaidii kwa kitu chochote kuwavumilia.


Musa akaandika maagizo yote ambayo Yawe alimupa. Kisha akaamuka asubui mapema, akajenga mazabahu chini ya mulima na kusimamisha nguzo kumi na mbili kulingana na hesabu ya makabila kumi na mbili ya Israeli.


Basi, kutakuwa mawe kumi na mawili yaliyochorwa majina kumi na mawili ya wana wa Israeli. Kila moja litakuwa kama muhuri, kwa kusimamia makabila yale kumi na mawili.


Basi, kulikuwa mawe kumi na mawili yaliyochorwa juu yake majina kumi na mawili ya wana wa Israeli. Yalikuwa yamechorwa kama vile wanavyochora muhuri, juu ya kila moja kulichorwa jina kwa ukumbusho wa makabila kumi na mawili.


Nitakapowasambaza kati ya mataifa mengine na inchi za mbali, halafu watatambua kwamba mimi ni Yawe.


Nitawatawanya ninyi kati ya watu wa mataifa na kuchomoa upanga juu yenu. Inchi yenu itakuwa ni ukiwa na miji yenu uharibifu.


kisha Filipo na Bartolomayo, Toma na Matayo aliyekuwa mulipishaji wa kodi; Yakobo mwana wa Alfayo, na Tadeo;


Huyu si mwana wa yule seremala? Mama yake si Maria? Nao Yakobo, Yosefu, Simoni na Yuda si wandugu zake?


Yesu akawajibu: “Kweli ninawaambia: Katika ulimwengu mupya, Mwana wa Mutu atakapoikaa juu ya kiti chake cha kifalme chenye utukufu, ninyi kumi na wawili mulionifuata mutaikaa vilevile juu ya viti kumi na viwili vya kifalme kwa kuhukumu makabila kumi na mawili ya Waisraeli.


Andrea na Filipo, Bartolomayo, Matayo, Toma, Yakobo mwana wa Alfayo, Tadeo, Simoni wa kundi la Wazeloti


kusudi mupate kula na kunywa pamoja nami katika ufalme wangu. Mutaikaa vilevile juu ya viti vya kifalme, kwa kuhukumu makabila kumi na mawili ya Waisraeli.”


Matayo na Toma, Yakobo mwana wa Alfayo na Simoni (wa kikundi cha Wazeloti),


Kama mutu akitaka kunitumikia, anapaswa kunifuata, na hivi mutumishi wangu atakuwa popote nitakapokuwa. Mutu akinitumikia, Baba yangu atamupa heshima.


Wayuda wakaulizana hivi wao kwa wao: “Mutu huyu atakwenda wapi sisi tusipoweza kumwona? Ataenda kwa Wayuda waliosambazwa kati ya Wagriki na kuwafundisha Wagriki?


Walipofika katika muji wakapanda katika chumba cha gorofi walipokuwa wanazoea kukutanana. Na waliokuwa pale ni hawa: Petro, Yoane, Yakobo, Andrea, Filipo, Toma, Bartolomayo, Matayo, Yakobo mwana wa Alfayo, Simoni wa kikundi cha Wazeloti na Yuda mwana wa Yakobo.


Naye akawanyamazisha kwa kunyoosha mukono, kuwaelezea namna Bwana alivyomwondoa katika kifungo. Akawaambia tena: “Muwaelezee Yakobo na wandugu wengine waamini habari hizi.” Kisha Petro akaondoka na kwenda nafasi ingine.


Nao walipomaliza kusema, Yakobo akajibu, akisema: “Wandugu zangu, munisikilize!


Kwa maana tangu zamani Sheria ya Musa inasomwa kila siku ya Sabato katika nyumba za kuabudia na kuhubiriwa katika kila muji.”


Nao wakawatuma na barua iliyoandikwa hivi: “Sisi mitume na wazee wa kanisa na wandugu zenu, tunawasalimu ninyi wandugu zetu waamini wa mataifa mengine munaokuwa katika muji wa Antiokia na katika jimbo la Suria na la Kilikia.


Katika Yerusalema kulikaa Wayuda wamoja waliotoka katika inchi zote za dunia, nao walikuwa watu wenye kuogopa Mungu.


Kesho yake tukaenda pamoja na Paulo kwa Yakobo, na wazee wote wa kanisa walikuwa kule vilevile.


“Mimi Klaudio Lusia, ninakuandikia wewe muheshimiwa Liwali Feliki, pokea salamu zangu.


Makabila yetu kumi na mawili wanamwabudu Mungu usiku na muchana, kwa maana wanatumaini kuona utimilifu wa ile ahadi. Na ni kwa sababu ya tumaini lile, Ee mufalme, Wayuda wananishitaki.


Naye Saulo alikuwa amekubali kwamba Stefano anastahili kuuawa. Siku ile ile kanisa lililokuwa katika Yerusalema lilianza kupata mateso makubwa. Waamini wote walisambaa katika Yudea na Samaria, isipokuwa mitume tu.


Barua hii inatoka kwangu mimi Paulo, mutumishi wa Kristo Yesu, niliyeitwa na Mungu kuwa mutume na niliyewekwa kwa kazi ya kutangaza Habari Njema yake.


Sikumwona mutu mwingine isipokuwa tu Yakobo, ndugu ya Bwana.


Kwa maana mbele ya kufika kwa watu wamoja waliotumwa na Yakobo kule, yeye alizoea kula pamoja na watu wa mataifa mengine. Lakini watu wale walipofika, akajitenga na kuacha kula pamoja na watu wa mataifa mengine, kwa sababu ya kuogopa wale wanaolazimisha kutahiriwa.


Basi Yakobo, Petro na Yoane, waliohesabiwa kuwa waongozi wakubwa, walitambua neema ile niliyojaliwa na Mungu wakatupatia mukono, mimi na Barnaba kuwa kitambulisho cha ushirika. Hivi tukapatana kwamba sisi tutakwenda kuhubiri watu wa mataifa mengine na wao watakwenda kuhubiri Wayuda.


Yawe atawatawanya kati ya mataifa yote, kutoka pembe moja ya dunia mpaka nyingine na huko mutaitumikia miungu mingine ya miti na mawe, miungu ambayo ninyi wala wazee wenu hamukuijua.


hapo Yawe, Mungu wenu, atawarudishia mema yenu na kuwahurumia na kuwakusanya tena kutoka katika mataifa ambamo atakuwa amewatawanya.


Ningaliwaangamiza kabisa na kuwafanya wasikumbukwe tena na mutu yeyote,


Yawe atawatawanya kati ya mataifa mengine, na ni wachache tu wenu watakaobakia huko ambako Yawe atawafukuzia.


Barua hii inatoka kwangu mimi Paulo na kwa ndugu yetu Timoteo, sisi watumishi wa Yesu Kristo. Tunawaandikia watu wote wa Mungu wanaoungana na Yesu Kristo, wanaoishi Filipi, pamoja na wazee wa kanisa na wasaidizi.


Ufanye nguvu kufika mbele ya wakati wa baridi kali. Eubulo, Pude, Lino, Klaudia na wandugu wote waamini wanakusalimia.


Barua hii inatoka kwangu mimi Paulo, mutumishi wa Mungu na mutume wa Yesu Kristo. Mimi nimetumwa kwa kuongoza watu waliochaguliwa na Mungu wapate kumwamini na kutambua ukweli unaolingana na dini yetu.


Barua hii inatoka kwangu mimi Petro, mutume wa Yesu Kristo. Ninawaandikia ninyi muliochaguliwa na Mungu na ambao mulisambazwa, na munaoishi kama wakimbizi kule Ponto, Galatia, Kapadokia, Azia na Bitinia.


Barua hii inatoka kwangu mimi Simoni Petro, mutumishi na mutume wa Yesu Kristo. Ninawaandikia ninyi mulioshiriki pamoja nasi katika imani ile inayokuwa kubwa kwa njia ya haki ya Mungu wetu na Mwokozi Yesu Kristo.


Barua hii inatoka kwangu mimi Yuda, mutumishi wa Yesu Kristo na ndugu wa Yakobo. Ninawaandikia ninyi mulioitwa na Mungu Baba na munaoishi katika upendo wake na kulindwa kwa ajili ya Yesu Kristo.


Nikasikia hesabu ya watu waliopigwa chapa ya muhuri wa Mungu ilikuwa: elfu mia moja na makumi ine na ine kutoka makabila yote ya Waisraeli.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ