Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Waroma 9:3 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

3 Ingekuwa heri nilaaniwe na kutengwa na Kristo kwa ajili ya wandugu zangu wa damu,

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Waroma 9:3
27 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Naye Labani akasema: “Hakika, wewe ni jamaa yangu, damu moja nami!” Yakobo akakaa naye kwa muda wa mwezi mumoja.


Maana, ninaweza namna gani kuvumilia kuona watu wangu wanaangamizwa na wandugu zangu wanauawa?”


Lakini sasa, ninakuomba uwasamehe zambi yao. Ikiwa hautawasamehe, ninakusihi unifute mimi katika kitabu chako ambamo uliwaandika watu wako.


“Wandugu zangu, ninyi wazao wa Abrahamu na ninyi watu wa mataifa mengine munaokuwa hapa kwa kumwabudu Mungu, habari hii ya wokovu imetumwa kwetu!


Hata Kuhani Mukubwa pamoja na baraza lote la wasimamizi wa watu wanaweza kushuhudia kwamba ninasema kweli. Nilipata hata barua toka kwao iliyoandikwa kwa ajili ya wandugu Wayuda wa Damasiki. Nikaenda kule kusudi niwafunge waamini waliokuwa kule na kuwaleta mpaka Yerusalema wapate kuazibiwa.


Wakamwambia: “Sisi hatukupokea barua juu yako toka Yudea, wala ndugu Muyuda aliyefika huku kwa kutupasha habari, wala kusema ubaya juu yako.


Habari hiyo inaelekea Mwana wake ndiye Bwana wetu Yesu Kristo, ambaye alizaliwa kimwili katika uzao wa mufalme Daudi. Lakini kwa namna ya Roho Mutakatifu, alihakikishwa kwa uwezo kuwa yeye ni Mwana wa Mungu kwa njia ya kufufuka kwake.


Basi ninauliza: Mungu amewatupilia watu wake? Hapana hata kidogo! Maana kwa ngambo yangu, mimi ni Mwisraeli wa uzao wa Abrahamu, toka kabila la Benjamina.


Kwa sababu hii ninaweza kuwafanya watu wa taifa langu wawasikilie wivu, hata nipate kuwaokoa wamoja kati yao.


Munisalimie Herodio, mwanainchi mwenzangu. Munisalimie watu wanaoishi katika nyumba ya Narkiso, wanaomwamini Bwana.


Timoteo, mutumishi mwenzangu anawasalimia, nao Lukio, Yasoni, na Sosipateri, wanainchi wenzangu wanawasalimia vilevile.


Munisalimie wanainchi wenzangu Androniko na Yunia, waliofungwa pamoja nami katika kifungo. Wao wanasifiwa sana kati ya mitume, nao walikuwa katika Kristo mbele yangu.


mimi nina huzuni kubwa na uchungu usiokuwa na mwisho ndani ya moyo wangu.


Kwa sababu hii ninataka mufahamu kwamba hakuna mutu ambaye anaongozwa na Roho wa Mungu anayeweza kusema: “Yesu alaaniwe,” na hakuna mutu anayeweza kusema: “Yesu ni Bwana,” kama asipoongozwa na Roho Mutakatifu.


Kama mutu hamupendi Bwana, alaaniwe! Bwana wetu, kuja!


Kwa ngambo yangu, nitafurahi kutumia vyote ninavyokuwa navyo na kujitoa mimi mwenyewe, kwa ajili yenu. Ikiwa ninawapenda zaidi namna hii, hamupaswi kupungukiwa na upendo kwangu.


Lakini kama sisi wenyewe au malaika kutoka mbinguni, akiwahubiri ninyi Habari Njema inayokuwa mbalimbali na ile tuliyowahubiri, alaaniwe!


Tumekwisha kuwaambia mambo haya zamani, nami ninayarudilia tena: mutu akiwahubiri habari njema inayokuwa mbalimbali na ile muliyopokea, alaaniwe!


Lakini wale wanaotegemea kutimiza yale yanayoamuriwa na Sheria, wamelaaniwa. Kwa maana Maandiko Matakatifu yanasema: “Alaaniwe mutu yeyote asiyedumu katika yote yanayoandikwa katika hiki kitabu cha Sheria na kuyatii.”


Kristo alitukomboa toka laana ya Sheria, akijitwalia laana hiyo kwa ajili yetu. Kwa maana Maandiko Matakatifu yanasema: “Mutu yeyote anayetundikwa juu ya muti amelaaniwa.”


Ninyi watumwa, mutii wabwana wenu kwa woga na kutetemeka na kwa moyo wa ukweli kama vile munavyomutumikia Kristo.


maiti yake isiachwe juu ya muti usiku wote, lakini mutaizika siku hiyohiyo. Maana mutu aliyetundikwa amelaaniwa na Mungu nanyi hamutachafua inchi yenu muliyopewa na Yawe, Mungu wenu, ikuwe urizi wenu.


Siku ile, Waisraeli walisumbuliwa sana maana Saulo alikuwa amewaapiza watu akisema: “Alaaniwe mutu yeyote atakayekula chakula mbele jua kutua, na mbele sijajilipiza waadui zangu kisasi.” Kwa hiyo, siku yote, hakuna mutu aliyeonja chakula chochote.


Saulo akasema: “Mungu aniue ikiwa Yonatani hatauawa.”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ