Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Waroma 8:3 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

3 Mungu alitimiza mambo yale Sheria ya Musa iliyoshindwa kuyatimiza, kwa sababu ya ukosefu wa nguvu unaotokana na hali zaifu ya kimwili. Mungu alitoa hukumu juu ya zambi inayotawala mwili kwa kutuma mwana wake wa peke katika hali ya kimutu, mwenye hali zaifu ya zambi kwa ajili ya kuondoa zambi.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Waroma 8:3
28 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Basi, Musa akatengeneza nyoka wa shaba, akamutundika juu ya muti. Kila mutu aliyeumwa na nyoka alipomuangalia nyoka huyo wa shaba, alipona.


Mutatoa vilevile beberu mumoja kuwa sadaka kwa ajili ya zambi kwa kuwafanyia upatanisho.


Vilevile waliwatundika wanyanganyi wawili juu ya misalaba pamoja na Yesu, mumoja kwa upande wake wa kuume na mwingine kwa upande wa kushoto. [


Neno alifanywa kuwa mutu, naye akaishi kati yetu, akijaa neema na ukweli. Tuliona utukufu wake, utukufu ule Mwana wa pekee aliopewa na Baba.


Halafu wakubwa wa Wayuda wakamwita yule aliyekuwa kipofu kwa mara ya pili na kumwambia: “Sema ukweli mbele ya Mungu! Kwa ngambo yetu tunajua kwamba mutu yule ni mwenye zambi.”


Kwa sababu hakuna mutu atakayehesabiwa haki mbele ya Mungu kwa kuwa anatii Sheria, maana Sheria inamusaidia mutu tu kwa kutambua kwamba amefanya zambi.


Kwa maana tunajua kwamba ule utu wetu wa zamani ulitundikwa pamoja na Kristo, kusudi tusitawaliwe tena na hiyo tabia ya zambi na tusikuwe tena watumwa wa zambi.


Kwa maana ninajua kwamba hakuna kitu kizuri kinachokaa ndani yangu, ni kusema katika hali yangu ya kimwili. Ni hivi kwa sababu ninakuwa na utashi wa kufanya jambo jema, lakini sifikii kulifanya.


Yeye hakumwacha Mwana wake wa pekee, lakini alimutoa kwa ajili yetu sisi wote. Namna gani atakosa kutupatia vilevile vitu vyote kwa njia ya mwana wake?


Ingekuwa heri nilaaniwe na kutengwa na Kristo kwa ajili ya wandugu zangu wa damu,


Kwa maana Kristo alikuwa bila zambi, lakini Mungu alimubebesha muzigo wa zambi zetu, kusudi kwa njia yake tupate kuwa wenye haki mbele ya Mungu.


Kristo alitukomboa toka laana ya Sheria, akijitwalia laana hiyo kwa ajili yetu. Kwa maana Maandiko Matakatifu yanasema: “Mutu yeyote anayetundikwa juu ya muti amelaaniwa.”


Basi, ni kusema kwamba Sheria haipatani na ahadi za Mungu? Hapana, hata kidogo! Kama kungetolewa Sheria yenye uwezo wa kuleta uzima kwa watu, basi mutu angehesabiwa haki mbele ya Mungu kwa njia ya Sheria.


Alitupilia hivi vyote, akatwaa hali ya mutumwa. Akatwaa mufano wa mutu, naye akaonekana katika hali ya kimutu.


Lakini Kristo yeye alitoa sadaka moja tu inayofaa kwa milele kwa ajili ya usamehe wa zambi. Na kisha akaikaa na mamlaka kwa kuume kwa Mungu.


Kwa maana kwa njia ya sadaka moja aliyotoa, amewafanya wale aliowatakasa kuwa wakamilifu hata milele.


Basi kwa kuwa hao watoto ni wanadamu, wenye mwili na damu, Yesu vilevile alitwaa ile hali ya mwanadamu. Alifanya hivi kusudi kwa njia ya kufa kwake amwangamize Shetani aliyekuwa na uwezo wa kuleta lufu.


Kwa hiyo ilimupasa afanane na wandugu zake katika mambo yote, kusudi apate kuwa Kuhani Mukubwa anayekuwa mwenye huruma na mwaminifu katika kazi yake mbele ya Mungu, na kwa njia hiyo zambi za watu zisamehewe.


Kwa maana tuko na Kuhani Mukubwa asiyekosa kujua mwenyewe uzaifu wetu. Maana yeye alijaribiwa katika njia zote sawasawa na sisi, lakini hakufanya zambi.


Kristo yeye mwenyewe alibeba mizigo ya zambi zetu ndani ya mwili wake alipoteswa juu ya musalaba, kusudi tupate kuachana na zambi kabisa na kuishi maisha ya haki. Kwa ajili ya mapigo yake ninyi muliponyeshwa.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ