Viumbe hivyo vilipokwenda, magurudumu nayo yalikwenda; viliposimama, nayo yalisimama; vilipoinuka juu kutoka kwenye udongo, magurudumu nayo yaliinuka pamoja navyo. Maana roho wa vile viumbe vya ajabu ilikuwa katika magurudumu hayo.
Yesu akamujibu: “Kama ungejua kitu Mungu anachoweza kukupatia, na ni nani anayekuomba maji ya kunywa, wewe ndiwe ungemwomba, naye angekupa maji ya uzima.”
lakini yeyote atakayekunywa maji yale nitakayomupa, hatasikia kiu tena hata kidogo. Maji nitakayomupa yatakuwa ndani yake kama chemichemi inayotiririka maji ya uzima wa milele.”
Hivi kama vile zambi ilivyotawala na kuleta kifo, hivi vilevile neema ya Mungu itawale kwa njia ya haki na kuleta uzima wa milele, kwa njia ya Yesu Kristo Bwana wetu.
Lakini sasa kufuatana na vile mumewekwa huru toka utawala wa zambi na kugeuka watumwa wa Mungu, munapata faida ya kuishi katika utakatifu na kwa mwisho kupewa uzima wa milele.
lakini ndani ya mwili wangu ninaona sheria ingine ikipigana na mafikiri yangu. Nayo inanifanya mufungwa wa sheria ya zambi inayotumika ndani ya mwili wangu.
Nanyi wandugu zangu, ni hivi inavyokuwa kwa ngambo yenu. Kufuatana na maneno ya Sheria, ninyi vilevile mumekufa, kwa maana muliungana na mwili wa Kristo. Na sasa munakuwa wa mutu mwingine, ndiye yule aliyefufuka, kusudi tupate kufanya matendo yanayofaa katika kazi ya Mungu.
Kwa maana Mungu ndiye aliyetuwezesha kuwa watumishi wa agano jipya, lisilotokana na Sheria iliyoandikwa, lakini na Roho. Sheria iliyoandikwa inaleta kifo lakini Roho analeta uzima.
Maana kufuatana na Sheria hiyo, mimi nimekuwa kama mufu, na kifo kile kimesababishwa na Sheria. Imetokea vile kusudi nipate kuishi kwa ajili ya Mungu. Mimi nimekufa pamoja na Kristo juu ya musalaba.
Lakini mutu anayechunguza sheria kamilifu inayoweka watu huru na kuendelea kushikamana nayo, na si kuisikia tu na kisha kuisahau, lakini anaitimiza kabisa, mutu huyu atabarikiwa na Mungu katika shuguli zake.
Lakini nyuma ya zile siku tatu na nusu, pumzi ya uzima inayotoka kwa Mungu ikaingia ndani ya maiti zao, nao wakasimama. Na watu wote waliowaona wakashikwa na woga mukubwa.
Kisha yule malaika akanionyesha muto wa maji ya uzima wenye kungaa kama kioo, uliokuwa ukitiririka toka kwenye kiti cha kifalme cha Mungu na cha Mwana-Kondoo.