Lakini kifo kilitawala tangia wakati wa Adamu mpaka wakati wa Musa, hata juu ya wale wasiofanya zambi kwa kuvunja amri, sawa vile Adamu alivyofanya. Naye ni mufano wa yule aliyengojewa kuja.
Hivi, kwa njia ya ubatizo, tuliungana naye katika kufa na katika kuzikwa kwake, kusudi kama vile Kristo alivyofufuliwa kwa uwezo wenye utukufu wa Baba, sisi vilevile tupate kuishi katika maisha mapya.
Ni kwa sababu hii anaweza kuwaokoa kabisa wao wanaokuja kwa Mungu kwa njia yake, kwa maana yeye anaishi siku zote kusudi akuwe mwombezi mbele ya Mungu.