Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Waroma 6:3 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

3 Munajua hakika kwamba sisi wote tulipobatizwa tuliungana na Yesu Kristo; kwa njia hiyo tuliungana naye katika kufa.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Waroma 6:3
24 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Basi muwaendee watu wa mataifa yote kusudi wapate kuwa wanafunzi wangu, mukiwabatiza kwa jina la Baba, la Mwana na la Roho Mutakatifu.


Waliposikia maneno haya, walibatizwa kwa jina la Bwana Yesu.


Petro akawajibu: “Mugeuke toka katika zambi zenu, na kila mumoja wenu abatizwe kwa jina la Yesu Kristo, na Mungu atawasamehe zambi zenu. Hivi mutapokea zawadi ya Roho Mutakatifu.


Kwa maana Roho Mutakatifu alikuwa bado hajashuka hata juu ya mumoja wao; walikuwa tu wamebatizwa kwa jina la Bwana Yesu.


Munajua hakika kwamba mukijitoa wenyewe kwa mutu fulani kuwa watumwa wake na kulazimishwa kumutii, munakuwa kweli watumwa wa yule munayemutii. Ikiwa ni utumwa wa zambi, mwisho wake ni kifo; ikiwa ni kumutii Mungu, mwisho wake ni maisha ya haki.


Ikiwa tumekufa pamoja na Kristo, tunaamini kwamba tutaishi pamoja naye vilevile.


Wandugu zangu, munajua uhakika juu ya maneno haya nitakayowaambia, kwa maana ninyi ni watu wanaoelewa Sheria vizuri: Sheria haina mamlaka juu ya mutu isipokuwa tu wakati angali muzima.


Wote walibatizwa katika lile wingu na katika ile bahari kusudi wapate kuungana na Musa.


Vilevile sisi wote, Wayuda na watu wa mataifa mengine, watumwa na watu wanaokuwa huru, tumebatizwa kwa Roho mumoja kusudi tukuwe mwili mumoja na sisi wote tumekunyweshwa Roho mumoja.


Ikiwa hakuna ufufuko, wale wanaobatizwa kwa ajili ya wafu watafanya nini? Ikiwa wafu hawafufuki kabisa, kwa sababu gani watu wanabatizwa kwa ajili yao?


Hamujui hakika kuwa ninyi ni hekalu la Mungu na kuwa Roho wa Mungu anakaa ndani yenu?


Hamuna kitu cha kujivunia! Hamujui vizuri mufano unaosema kwamba chachu kidogo inachachisha donge zima?


Hamujui kwamba mwili wenu ni hekalu la Roho Mutakatifu anayekuwa ndani yenu, yule muliyepewa na Mungu? Na ninyi si mali yenu wenyewe.


Ninyi munajua hakika kwamba watenda mabaya hawatapata urizi katika Ufalme wa Mungu. Musidanganyike: waasherati, wenye kuabudu sanamu, wazinzi, waasherati wa muke kwa muke na mume kwa mume,


Munajua hakika kuwa wale wanaotumika katika hekalu wanapata chakula chao ndani ya hekalu. Na wale wanaotumika kwa kutoa sadaka juu ya mazabahu wanapata sehemu yao kutoka sadaka zile.


Munajua hakika kuwa wale wanaofanya mashindano ya kukimbia, wote wanakimbia lakini ni mumoja tu anayepokea zawadi. Basi mukimbie hata mufikie kupokea zawadi.


Mujichunguze ninyi wenyewe kusudi mupate kujua kama munasimama imara katika imani. Mujipime. Si munajua kwamba Yesu Kristo anakaa kati yenu? Kama si vile ni kusema kwamba mumeshindwa.


Hivi, ninyi wote mulioungana na Yesu Kristo, kwa njia ya kubatizwa, ni kama vile mumevaa Kristo.


Ninyi watu wasiokuwa na uaminifu! Hamujui kwamba kupenda raha ya dunia ni kuwa adui wa Mungu? Basi yeye anayetaka kupenda raha za dunia anajifanya mwenyewe kuwa adui wa Mungu.


Maji haya ni mufano wa ubatizo unaowaokoa ninyi sasa. Ubatizo ule si kwa ajili ya kusafisha uchafu wa mwili lakini ni njia ya kufanya mapatano na Mungu katika zamiri safi. Nao unawaokoa ninyi kwa njia ya ufufuko wa Yesu Kristo,


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ