Hapa ndani ya nyumba yeye hana madaraka kuliko mimi. Yeye hakunikataza kushika chochote isipokuwa wewe tu kwa sababu wewe ni muke wake. Nitaweza namna gani basi kufanya uovu mubaya kama ule na kumukosea Mungu?”
Atakuja na kuwaua wale walimaji. Na kisha atawapatia walimaji wengine shamba lile.” Watu waliposikia maneno hayo, wakasema: “Isitufikie vile hata kidogo.”
Nanyi wandugu zangu, ni hivi inavyokuwa kwa ngambo yenu. Kufuatana na maneno ya Sheria, ninyi vilevile mumekufa, kwa maana muliungana na mwili wa Kristo. Na sasa munakuwa wa mutu mwingine, ndiye yule aliyefufuka, kusudi tupate kufanya matendo yanayofaa katika kazi ya Mungu.
Lakini sasa tumekuwa huru toka vifungo vya Sheria, kwa maana tunakuwa kama waliokufa kufuatana na mambo yale yaliyotufunga. Kwa hiyo tunaweza kumutumikia Mungu kwa kufuata njia mupya chini ya uongozi wa Roho wake, wala si kufuata njia ya zamani chini ya uongozi wa maandiko ya Sheria.
Maana kufuatana na Sheria hiyo, mimi nimekuwa kama mufu, na kifo kile kimesababishwa na Sheria. Imetokea vile kusudi nipate kuishi kwa ajili ya Mungu. Mimi nimekufa pamoja na Kristo juu ya musalaba.
Na mimi kwa ngambo yangu sitaki kujivuna, isipokuwa tu kwa ajili ya musalaba wa Bwana wetu Yesu Kristo. Maana kwa njia ya musalaba huo, ninahesabu dunia kama vile imekwisha kufa na mbele ya dunia mimi ninahesabiwa kama vile mufu.
Ninyi mumekufa pamoja na Kristo na kukombolewa toka katika uwezo wa roho mbaya zinazotawala dunia. Kwa nini munaishi tena kama watu wa dunia mukilazimishwa kushika kanuni kama hizi:
Kristo yeye mwenyewe alibeba mizigo ya zambi zetu ndani ya mwili wake alipoteswa juu ya musalaba, kusudi tupate kuachana na zambi kabisa na kuishi maisha ya haki. Kwa ajili ya mapigo yake ninyi muliponyeshwa.