Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Waroma 6:2 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

2 Hapana hata kidogo! Sisi tuliokufa kwa ajili ya zambi, namna gani tutaweza tena kuishi katika zambi?

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Waroma 6:2
18 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Hapa ndani ya nyumba yeye hana madaraka kuliko mimi. Yeye hakunikataza kushika chochote isipokuwa wewe tu kwa sababu wewe ni muke wake. Nitaweza namna gani basi kufanya uovu mubaya kama ule na kumukosea Mungu?”


Kwa kanuni zako ninapata hekima, kwa hiyo ninachukia kila mwenendo mubaya.


Atakuja na kuwaua wale walimaji. Na kisha atawapatia walimaji wengine shamba lile.” Watu waliposikia maneno hayo, wakasema: “Isitufikie vile hata kidogo.”


Wala si ile tu, lakini tunafurahi kwa ajili ya Mungu kwa njia ya Bwana wetu Yesu Kristo aliyetupatanisha sasa na Mungu.


Ni nini basi? Tufanye zambi kwa sababu sisi hatuishi chini ya Sheria, lakini chini ya uwongozi wa neema ya Mungu? Hapana hata kidogo!


Nanyi wandugu zangu, ni hivi inavyokuwa kwa ngambo yenu. Kufuatana na maneno ya Sheria, ninyi vilevile mumekufa, kwa maana muliungana na mwili wa Kristo. Na sasa munakuwa wa mutu mwingine, ndiye yule aliyefufuka, kusudi tupate kufanya matendo yanayofaa katika kazi ya Mungu.


Lakini sasa tumekuwa huru toka vifungo vya Sheria, kwa maana tunakuwa kama waliokufa kufuatana na mambo yale yaliyotufunga. Kwa hiyo tunaweza kumutumikia Mungu kwa kufuata njia mupya chini ya uongozi wa Roho wake, wala si kufuata njia ya zamani chini ya uongozi wa maandiko ya Sheria.


Maana kufuatana na Sheria hiyo, mimi nimekuwa kama mufu, na kifo kile kimesababishwa na Sheria. Imetokea vile kusudi nipate kuishi kwa ajili ya Mungu. Mimi nimekufa pamoja na Kristo juu ya musalaba.


Na mimi kwa ngambo yangu sitaki kujivuna, isipokuwa tu kwa ajili ya musalaba wa Bwana wetu Yesu Kristo. Maana kwa njia ya musalaba huo, ninahesabu dunia kama vile imekwisha kufa na mbele ya dunia mimi ninahesabiwa kama vile mufu.


Ninyi mumekufa pamoja na Kristo na kukombolewa toka katika uwezo wa roho mbaya zinazotawala dunia. Kwa nini munaishi tena kama watu wa dunia mukilazimishwa kushika kanuni kama hizi:


Kwa maana ninyi mumekufa na uzima wenu umefichwa pamoja na Kristo katika Mungu.


Kama watoto wenye utii, musiachilie maisha yenu kutawaliwa na tamaa mbaya mulizokuwa nazo zamani wakati mulipokuwa mukiishi katika ujinga.


Kristo yeye mwenyewe alibeba mizigo ya zambi zetu ndani ya mwili wake alipoteswa juu ya musalaba, kusudi tupate kuachana na zambi kabisa na kuishi maisha ya haki. Kwa ajili ya mapigo yake ninyi muliponyeshwa.


Kila mutu anayekuwa mutoto wa Mungu hafanyi zambi, kwa sababu neno la Mungu linakaa ndani yake; tena hawezi kufanya zambi, maana Mungu ni baba yake.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ