Wao walijitolea kufa kwa kuokoa maisha yangu. Ninawashukuru, wala si mimi peke yangu tu, nayo makanisa yote ya inchi za watu wa mataifa wanawashukuru vilevile.
Yule mulinzi akasema: “Ninaona kwamba yule anayekimbia zaidi ni Ahimasi mwana wa Zadoki.” Mufalme akasema: “Huyo ni mutu muzuri, anatuletea habari njema.”
Lakini watu wakamwambia: “Hautakwenda. Maana, ikiwa tutakimbia, hawatajali kitu juu yetu. Ikiwa nusu yetu watakufa, hawatahangaika nasi vilevile. Lakini wewe ni wa lazima kuliko watu elfu kumi kati yetu. Kwa hiyo inafaa wewe ubaki katika muji na kutupelekea musaada ukiwa katika muji.”