Na si viumbe hivi tu; hata sisi tuliokwisha kuwa na Roho wa Mungu kama sehemu ya kwanza ya zawadi Mungu atakazotoa, tunaugua vilevile ndani yetu, tukingojea kukubaliwa na Mungu kuwa watoto wake, maana yake kukombolewa kwa kimwili.
Vilevile, yule ndugu amechaguliwa na makanisa kwa kutusindikiza katika safari ya kutimiza kazi hii ya kutoa kwa moyo mwema ambayo sisi tunafanya kwa ajili ya utukufu wa Bwana, na kwa kuonyesha nia yetu ya kusaidia watu wengine.
Heri mutu yule anayevumilia wakati anapojaribiwa, kwa maana akiisha kushinda majaribu, atapokea ile taji ya uzima ambayo Mungu aliahidia wale wanaomupenda.