Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Waroma 5:2 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

2 Kwa njia ya imani, Yesu ametuwezesha kukaribia neema ya Mungu, inayokuwa musingi wetu. Sababu hii tunafurahi tukiwa na tumaini la kushiriki katika utukufu wa Mungu.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Waroma 5:2
43 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Lakini mimi nitauona uso wako, maana mimi ni mutu wa haki; nitakapoamuka nitajaa furaha kwa sababu unanitokea.


Wewe unaniongoza kwa mashauri yako; na kwa mwisho utanipokea kwenye utukufu.


Mwovu anaangamizwa kwa matendo yake maovu, lakini mwenye haki atapata usalama kwa uaminifu wake.


mimi nitaendelea kumufurahia Yawe. Nitamushangilia Mungu anayeniokoa.


Bwana wake akamwambia: ‘Ni vizuri, wewe mutumishi mwema na mwaminifu. Ulikuwa mwaminifu katika ulinzi wa mali ndogo, basi nitakuweka kuwa mulinzi wa mali mengi. Kuja ufurahi pamoja na bwana wako.’


Basi Yesu akaongeza kusema: “Kweli, kweli ninawaambia: mimi ni mulango wa upango wa kondoo.


Mimi ni mulango. Mutu akiingia kwa kupitia kwangu, ataokoka, ataingia na kutoka, naye atapata chakula.


Yesu akamujibu: “Mimi ni njia, ukweli na uzima. Mutu hawezi kufika kwa Baba asipopitia kwangu.


“Kweli, kweli ninawaambia: anayesikia neno langu na kumwamini yule aliyenituma, anapata uzima wa milele. Yeye hatahukumiwa, lakini ameponyoka lufu na kupata uzima.


Walipofika Antiokia, wakafanya mukutano wa kanisa na kuwaelezea mambo yote Mungu aliyofanya kwa njia yao, na namna alivyowafungulia watu wa mataifa mengine mulango kusudi wao vilevile wapate kuamini.


Unasema ukweli. Yamekatwa kwa sababu yalikataa kuamini na wewe unasimama imara katika imani yako. Sasa usijivune, lakini uogope!


Mufurahi mukiwa na tumaini, muvumilie katika mateso, mudumu katika kuomba.


Wewe ni nani unayehukumu mutumishi wa mwingine? Akisimama imara katika kazi yake au akianguka, hilo ni shauri la bwana wake. Naye atasimama imara maana Bwana yuko na uwezo wa kumusimamisha.


Basi, Mungu anayekuwa musingi wa matumaini, awajaze furaha kamili na amani kutokana na imani yenu; hata tumaini lenu lipate kuongezeka kwa nguvu ya Roho Mutakatifu.


Wale wanaofanya matendo mema bila kuchoka na kutafuta toka kwa Mungu utukufu, heshima na uzima usiokuwa na mwisho, Mungu atawapa uzima wa milele.


kwa maana wote wamefanya zambi na kukosa utukufu wa Mungu.


Nalo tumaini hili si la udanganyifu, kwa sababu Mungu amemimia upendo wake ndani ya mioyo yetu kwa njia ya Roho Mutakatifu aliyetupatia.


Basi sasa hakuna azabu kwa wale wanaoungana na Yesu Kristo.


Kwa maana tumeokolewa, lakini ni kwa tumaini. Mutu akiona kitu anachokitumainia, hilo si tumaini tena, kwa maana nani anayeweza kuendelea kutumainia kitu anachokiona?


Wandugu zangu, sasa ninataka kuwakumbusha Habari Njema niliyowatangazia, ile muliyopokea na kuishika imara.


Sisi wote ambao uso haukufunikwa, tunaonyesha kama kioo utukufu wa Bwana. Kwa hiyo, tunabadilishwa kwa kufanana na Bwana, nasi tunapita toka utukufu mumoja hata utukufu mwingine unaokuwa mukubwa zaidi tena. Kwa maana kazi hii inatimizwa na Bwana ndiye Roho.


Kwa maana taabu tunayopata ni ndogo na ya muda tu, inatutayarishia utukufu mukubwa sana na wa milele unaokuwa muzuri zaidi kupita mateso haya.


Kwa maana, kwa njia ya Kristo sisi wote, Wayuda na watu wa mataifa mengine, tumefunguliwa njia ya kufika mbele ya Baba katika Roho mumoja.


Na katika kuungana kwetu na Yesu Kristo na kwa njia ya kumwamini tunapata uhuru wa kufika mbele ya Mungu tukiwa na tumaini kubwa.


Kwa hiyo sasa mutwae silaha zote Mungu anazowapatia. Kwa njia hii mutaweza kushinda adui yenu siku mbaya itakapowafikia. Nanyi mutakapokwisha kumaliza mapigano, mutaweza kusimama imara.


Bwana wetu Yesu Kristo mwenyewe na Mungu Baba yetu, aliyetupenda na kwa neema yake akatufariji kwa milele na kutupatia tumaini njema,


Lakini Kristo ni mwaminifu kama Mwana anayesimamia nyumba ya Mungu. Na sisi ndio nyumba ile, kama tukiendelea kuwa na uhodari na kuaminia kupata mambo tunayotumainia.


Basi kuna mambo mawili, ahadi na kiapo, yasiyoweza kubadilika, na kuelekea hayo, Mungu hawezi kusema uongo. Kwa hivi, sisi tuliomukimbilia tunatiwa moyo sana na kushika kwa nguvu tumaini tulilowekewa.


Kufuatana na hiyo, Kristo naye alikufa mara moja tu kwa sababu ya zambi zenu. Yeye alikuwa mwenye haki kwa ajili ya waovu, kusudi awaonyeshe ninyi njia ya kumufuata Mungu. Aliuawa kimwili, lakini kwa uwezo wa Roho Mutakatifu alipata tena uzima.


nao ukingaa kwa utukufu wa Mungu. Mwangaza wake ulikuwa kama jiwe la bei kali la yaspi, linalongaa kama kioo.


Muji ule hauna lazima ya mwangaza wa jua, wala wa mwezi, kwa sababu utukufu wa Mungu unauangazia na Mwana-Kondoo ndiye taa yake.


Nikasikia sauti kubwa tokea kwenye kiti cha kifalme ikisema: “Sasa makao ya Mungu yanapatikana kati ya watu! Yeye atakaa pamoja nao, nao watakuwa watu wake. Mungu mwenyewe atakuwa pamoja nao, naye atakuwa Mungu wao.


Yule atakayeshinda, nitamwikalisha karibu nami kwenye kiti changu cha kifalme, kama vile mimi nilivyoshinda na kuikaa karibu na Baba yangu kwenye kiti chake cha kifalme.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ