Mungu hakuwakataa watu wake aliojichagulia tangu mbele. Munakumbuka Maandiko Matakatifu yanayosema juu ya mashitaki ya Elia mbele ya Mungu juu ya Waisraeli? Yeye alisema:
Nyuma ya pale alitahiriwa, na kutahiriwa kwake kulikuwa kitambulisho cha kuhakikisha ile haki Mungu aliyomuhesabia kwa njia ya imani yake. Hivi Abrahamu akakuwa baba wa watu wote wanaoamini, ijapokuwa hawatahiriwi, kusudi wao vilevile wahesabiwe haki.
Uheri huu si kwa watu wanaotahiriwa tu, lakini ni kwa watu wasiotahiriwa vilevile. Kwa maana tumekwisha kusema kwamba Abrahamu alihesabiwa kuwa mwenye haki kwa njia ya imani yake.
Mungu anamwambia mufalme wa Misri katika Maandiko Matakatifu: “Nimekusimika kuwa mufalme kwa sababu hii moja, ni kusudi kwa njia yako nipate kuonyesha uwezo wangu na kusudi jina langu lipate kutangazwa katika dunia yote.”