Ni nani aliyekuweka kuwa mukubwa kuliko wengine? Si Mungu ndiye aliyekupa vitu vyote unavyokuwa navyo? Ikiwa ni hivi, kwa sababu gani unajivuna kama vile haukuvipewa kama zawadi?
Sisi hatuanzi tena kujisifu wenyewe mbele yenu, lakini tunawapa ninyi sababu ya kuweza kujivuna kwa ajili yetu. Hivi tena munaweza kupata maneno ya kuwajibu wale wanaojivunia tu hali yao ya inje, lakini si mambo yanayokuwa ndani ya mioyo yao.
Lakini Maandiko Matakatifu yanasema kwamba watu wote wako chini ya utumwa wa zambi, kusudi zawadi iliyoahidiwa na Mungu itolewe kwa wale wanaoamini kwa njia ya imani yao katika Yesu Kristo.
na kuungana naye kabisa. Nami sihesabiwi haki tena kufuatana na mambo niliyofanya, ndiyo ile haki inayopatikana kwa njia ya kushika Sheria. Lakini ninahesabiwa haki kwa njia ya kumwamini Kristo, ndiyo ile haki inatoka kwa Mungu, naye anamuhesabia haki yule anayeamini.
Yoshua akawaambia watu wote: “Yawe, Mungu wa Israeli, anasema hivi: Hapo zamani, wazee wenu waliishi ngambo ya muto Furati, wakaitumikia miungu mingine. Muzee mumoja aliitwa Tera, baba ya Abrahamu na Nahori.