10 Na tena Maandiko yanasema: “Ninyi watu wa mataifa yote mufurahi pamoja na taifa lake!”
Wajumbe watakuja kutoka Misri, Waetiopia watamuletea Mungu mali zao.
Yawe anatawala! Furahi, ee dunia! Mufurahi, enyi visanga vingi!
Mushangilie na kufurahi pamoja na Yerusalema, enyi munaoupenda! Mushangilie pamoja nao, enyi wote mulioulilia!
Enyi mataifa, mushangilie watu wake, maana yeye analipiza kisasi damu ya watumishi wake, anawalipiza kisasi wapinzani wake, na kuitakasa inchi ya watu wake.