Waroma 13:9 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
9 Kwa hiyo amri hizi: “Usizini, usiue, usiibe, usitamani,” pamoja na zingine zote, zinafungwa katika amri hii moja: “Umupende mwenzako sawa vile unavyojipenda mwenyewe.”
Huyo mugeni anayekaa nawe atakuwa kwako kama vile mwenyeji nawe utamupenda kama vile unavyojipenda mwenyewe, kwa sababu nawe ulikuwa mugeni katika inchi ya Misri. Mimi ni Yawe, Mungu wenu.
Mutu yule akamujibu kwa maneno haya: “ ‘Umupende Bwana Mungu wako kwa moyo wako wote, kwa roho yako yote, kwa nguvu yako yote na kwa akili yako yote.’ Vilevile, ‘Umupende mwenzako kama vile unavyojipenda mwenyewe.’ ”
Wandugu, ninyi muliitwa na Mungu kusudi mukuwe watu huru. Basi musitumie uhuru huu kuwa ruhusa ya kutimiza tamaa za mwili, lakini musaidiane kwa upendo.