Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Waroma 13:4 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

4 maana yeye anamutumikia Mungu kwa faida yako. Lakini kama ukifanya mabaya, umwogope kwa sababu yeye yuko na uwezo kwa kuazibu. Yeye anamutumikia Mungu wa kuazibu wale wanaofanya mabaya.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Waroma 13:4
23 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Wandugu wapendwa, musilipize kisasi ninyi kwa ninyi, lakini mumwachie Mungu wakati wa kutenda kufuatana na kasirani, maana imeandikwa katika Maandiko Matakatifu: “Ni kazi yangu kulipiza kisasi. Ni mimi nitakayelipiza.”


Kasirani kali ya mufalme ni kama simba anayenguruma; anayemukasirikisha anahatarisha maisha yake.


Hasira ya mufalme ni kama mujumbe wa kifo; mutu mwenye hekima ataituliza.


akawaambia: “Muwe waangalifu sana wakati munapoamua, kwa maana hukumu munayotoa hamuitoi kwa amri ya mwanadamu, lakini kwa amri inayotoka kwa Yawe, naye yuko pamoja nanyi munapotoa uamuzi.


Kuelekea maneno hayo, mutu yeyote asimukosee ndugu yake wala kumudanganya. Tumekwisha kuwaambia na kuwahakikishia mbele kwamba Bwana atawaazibu wale wanaofanya mambo kama hayo.


Kwa sababu hii vilevile munalipa kodi, maana watawala wanamutumikia Mungu wakijitoa kwa kazi ile.


Musikie jambo hili, enyi waongozi wa wazao wa Yakobo, musikilize, enyi watawala wa Waisraeli: Ninyi munachukia sheria ya Mungu na kupotosha mambo ya usawa.


Nitawafanya watu wangu Waisraeli walipize kisasi juu ya Waedomu nao watawatendea Waedomu kadiri ya hasira na kasirani yangu. Halafu Waedomu watatambua uzito wa kisasi changu. –Ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe.


Wakubwa wake wanaokuwa ndani ya muji ni kama imbwa wa pori wanaorarua nyama wao; wanaua kwa kujitajirisha kwa namna isiyokuwa ya haki.


wamenenepa na kungaa vizuri. Maovu yao hayana mwisho, hawahukumu yatima kwa kufuatana na sheria kusudi wapate kufanikiwa, wala hawatetei haki za watu wakosefu.


mujifunze kutenda mema. Mufuate sheria ya Mungu, mumusaidie mwenye kuteswa, mumupatie yatima haki yake, mutetee haki za wajane.


Mufalme mwenye hekima anapepeta waovu; anawaazibu bila huruma.


Mufalme anapoikaa kwa kutoa hukumu, anapepeta uovu wote kwa macho yake.


Asifiwe Yawe, Mungu wako, ambaye amependezwa nawe, akakuweka juu ya kiti cha kifalme cha Israeli! Kwa sababu Yawe anapenda Israeli milele, amekuweka wewe ukuwe mufalme, kusudi uimarishe haki na sheria ya Mungu.”


Hii ndiyo miji iliyotengwa kwa ajili ya watu wote wa Israeli na wageni walioishi kati yao, kusudi mutu yeyote atakayemwua mwenzake bila kukusudia akimbilie kule asipate kuuawa na mwenye ruhusa ya kulipiza kisasi cha damu, mpaka pale atakapohukumiwa mbele ya mukutano wa watu wote.


Kama yule mutu mwenye kuwa na ruhusa ya kulipiza kisasi akimufuatilia mpaka katika muji ule, wazee wa muji ule hawaruhusiwi kumutoa mwuaji yule kwa yule mwenye kutaka kulipiza kisasi maana alimwua mwenzake kwa bahati mbaya tu kwa vile hakukukuwa uadui kati yao zamani.


au ikiwa maliwali waliosimikwa naye kwa kuwaazibu watenda mabaya na kuwapa zawadi wale wanaotenda mema.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ