7 Wala usijiulize: “Ni nani atakayeshuka katika kuzimu?” (maana yake kumupandisha Kristo toka kule kwenye wafu).
Nao wale pepo walimusihi Yesu kwamba atakapowafukuza asiwaamuru kutumbukia ndani ya shimo lisilokuwa na mwisho.
Alitolewa kufa sababu ya makosa yetu na kufufuliwa kusudi tupate kuhesabiwa haki mbele ya Mungu.
Mungu wa amani, aliyemufufua Bwana wetu Yesu ambaye ni Muchungaji mukubwa wa kondoo kwa njia ya kumwanga damu yake inayohakikisha agano la milele,
Kufuatana na hiyo, Kristo naye alikufa mara moja tu kwa sababu ya zambi zenu. Yeye alikuwa mwenye haki kwa ajili ya waovu, kusudi awaonyeshe ninyi njia ya kumufuata Mungu. Aliuawa kimwili, lakini kwa uwezo wa Roho Mutakatifu alipata tena uzima.
aliyepanda mbinguni, na anayekaa na mamlaka kwa kuume kwa Mungu, akitawala wamalaika, nao wenye mamlaka na uwezo wanaokuwa katika mbingu.
Mimi ni mwenye uzima. Nilikuwa nimekufa, lakini sasa mimi niko muzima kwa milele na milele. Niko na mamlaka juu ya lufu na kuzimu.