Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Waroma 10:3 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

3 Hawakufahamu namna Mungu anavyowahesabia watu haki na wakatafuta kusimamisha haki yao wenyewe. Wakakataa kufuata njia ya kuhesabiwa haki mbele ya Mungu.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Waroma 10:3
34 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Hata hivyo, una haki kwa kutuazibu hivyo; maana wewe umekuwa mwaminifu wakati sisi tumekuwa watenda maovu.


Atashangilia mbele ya watu na kusema: “Nilitenda zambi na kupotosha usawa, nami sikuazibiwa kutokana na hayo.


Nguvu na haki yako, ee Mungu, vinafika mpaka juu katika mbingu. Wewe umefanya mambo makubwa sana. Ee Mungu, ni nani anayekuwa kama wewe?


Yawe anasema hivi: Munisikilize enyi munaotaka kukombolewa, ninyi munaonitafuta mimi Yawe. Muangalie jiwe mulilochongwa toka ndani yake, mulima mulimochimbuliwa.


Muinue macho, muangalie mbingu, kisha muangalie dunia kule chini. Mbingu zitatoweka kama moshi, dunia itachakaa kama nguo, na wakaaji wake watakufa kama vidudu. Lakini wokovu ninaouleta unadumu milele; ukombozi wangu hautakoma hata kidogo.


Maana watakuliwa na nondo kama vile nguo; vidudu watawakula kama wanavyokula nguo ya manyoya ya kondoo. Lakini ukombozi ninaouleta mimi utadumu milele; wokovu wangu hautakuwa na mwisho.


Yawe anasema hivi: Mufuate sheria yangu na kutenda kwa haki, maana ninakaribia kuwaokoa, watu wataona wazi kwamba ninawakomboa.


Munafikiri kwamba munafanya sawa, lakini nitayafichua matendo yenu, nayo miungu yenu haitawafalia kitu.


Hakuna hata mumoja anayekuja kukuomba; hakuna anayejishugulisha kukutafuta. Wewe unauficha uso wako mbali nasi, umetuacha tufungwe na maovu yetu.


Wema wa Yawe haukomi, huruma zake hazina mwisho.


Muda wa miaka saba mara makumi saba umewekwa kwa ajili ya watu wako na juu ya muji wako mutakatifu kwa kumaliza makosa, kukomesha zambi, kusamehe uovu, kuleta haki ya milele, kutia muhuri juu ya maono na unabii na kupakaa mafuta katika Pahali Patakatifu Sana.


wakitambua kwa nini nilipingana nao na kuwapeleka katika inchi ya waadui zao, kama kweli moyo wao mugumu ukinyenyekea na kutubu uovu wao,


Lakini kwa kutaka kujipatia haki, yeye akamwuliza Yesu: “Mwenzangu ni nani?”


Yesu akawaambia: “Ninyi ni watu wanaojionyesha kuwa wenye haki mbele ya watu, lakini Mungu anajua yanayokuwa ndani ya mioyo yenu. Kwa maana mambo yanayosifiwa na watu ni machukizo mbele ya Mungu.


Kwa maana Habari Njema inaonyesha namna Mungu anavyowahesabia watu haki mbele yake. Jambo hilo haliwezekani isipokuwa kwa njia ya kuamini tu. Ni sawa vile inavyoandikwa katika Maandiko Matakatifu yanayosema: “Mwenye haki ataishi kwa njia ya imani.”


Kwa maana ninashuhudia kwamba wanajitoa kwa bidii kutumikia Mungu, lakini bidii ile haitokani na ufahamu wa kweli.


Isaya kwa uhodari anaongeza kusema maneno haya: “Nimepatikana kwa watu wasionitafuta, nimejifunua kwa watu wasioniuliza.”


Nini basi? Taifa la Waisraeli halikupata kile walichokitafuta. Ni wachache tu ambao Mungu aliwachagua ndio waliokipata. Lakini wengine waliobaki, walifanywa kuwa wagumu,


kuhesabiwa haki na Mungu kunapatikana kwa njia ya imani katika Yesu Kristo kwa wote wanaoamini, kwa maana hakuna tofauti yoyote kati yao,


Na kama vile kutokana na uasi wa mutu mumoja, watu wengi wamekuwa wenye zambi, ni hivi vilevile kutokana na utii wa mutu mumoja, watu wengi watahesabiwa haki mbele ya Mungu.


Kwa maana Kristo alikuwa bila zambi, lakini Mungu alimubebesha muzigo wa zambi zetu, kusudi kwa njia yake tupate kuwa wenye haki mbele ya Mungu.


Tukiwa waangalifu tukitimiza amri zote mbele ya Yawe, Mungu wetu, kama vile alivyotuamuru, tutahesabiwa kuwa wenye haki’.


na kuungana naye kabisa. Nami sihesabiwi haki tena kufuatana na mambo niliyofanya, ndiyo ile haki inayopatikana kwa njia ya kushika Sheria. Lakini ninahesabiwa haki kwa njia ya kumwamini Kristo, ndiyo ile haki inatoka kwa Mungu, naye anamuhesabia haki yule anayeamini.


Barua hii inatoka kwangu mimi Simoni Petro, mutumishi na mutume wa Yesu Kristo. Ninawaandikia ninyi mulioshiriki pamoja nasi katika imani ile inayokuwa kubwa kwa njia ya haki ya Mungu wetu na Mwokozi Yesu Kristo.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ