Waroma 10:3 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
3 Hawakufahamu namna Mungu anavyowahesabia watu haki na wakatafuta kusimamisha haki yao wenyewe. Wakakataa kufuata njia ya kuhesabiwa haki mbele ya Mungu.
Muinue macho, muangalie mbingu, kisha muangalie dunia kule chini. Mbingu zitatoweka kama moshi, dunia itachakaa kama nguo, na wakaaji wake watakufa kama vidudu. Lakini wokovu ninaouleta unadumu milele; ukombozi wangu hautakoma hata kidogo.
Maana watakuliwa na nondo kama vile nguo; vidudu watawakula kama wanavyokula nguo ya manyoya ya kondoo. Lakini ukombozi ninaouleta mimi utadumu milele; wokovu wangu hautakuwa na mwisho.
Muda wa miaka saba mara makumi saba umewekwa kwa ajili ya watu wako na juu ya muji wako mutakatifu kwa kumaliza makosa, kukomesha zambi, kusamehe uovu, kuleta haki ya milele, kutia muhuri juu ya maono na unabii na kupakaa mafuta katika Pahali Patakatifu Sana.
Yesu akawaambia: “Ninyi ni watu wanaojionyesha kuwa wenye haki mbele ya watu, lakini Mungu anajua yanayokuwa ndani ya mioyo yenu. Kwa maana mambo yanayosifiwa na watu ni machukizo mbele ya Mungu.
Kwa maana Habari Njema inaonyesha namna Mungu anavyowahesabia watu haki mbele yake. Jambo hilo haliwezekani isipokuwa kwa njia ya kuamini tu. Ni sawa vile inavyoandikwa katika Maandiko Matakatifu yanayosema: “Mwenye haki ataishi kwa njia ya imani.”
Nini basi? Taifa la Waisraeli halikupata kile walichokitafuta. Ni wachache tu ambao Mungu aliwachagua ndio waliokipata. Lakini wengine waliobaki, walifanywa kuwa wagumu,
Na kama vile kutokana na uasi wa mutu mumoja, watu wengi wamekuwa wenye zambi, ni hivi vilevile kutokana na utii wa mutu mumoja, watu wengi watahesabiwa haki mbele ya Mungu.
na kuungana naye kabisa. Nami sihesabiwi haki tena kufuatana na mambo niliyofanya, ndiyo ile haki inayopatikana kwa njia ya kushika Sheria. Lakini ninahesabiwa haki kwa njia ya kumwamini Kristo, ndiyo ile haki inatoka kwa Mungu, naye anamuhesabia haki yule anayeamini.
Barua hii inatoka kwangu mimi Simoni Petro, mutumishi na mutume wa Yesu Kristo. Ninawaandikia ninyi mulioshiriki pamoja nasi katika imani ile inayokuwa kubwa kwa njia ya haki ya Mungu wetu na Mwokozi Yesu Kristo.