Nyuma ya mambo yale, Paulo alikusudia kwenda Yerusalema, akipitia katika inchi ya Makedonia na katika jimbo la Akaya. Akasema: “Nikisha kufika kule, ni lazima niende Roma vilevile.”
Lakini ninakubali mbele yako kwamba ninamutumikia Mungu wa babu zetu nikifuata Njia ile wanayosema kwamba ni ya uongo. Mimi ninaamini maneno yote yaliyoandikwa katika kitabu cha Sheria na katika vitabu vya manabii.
Munajua ninyi wenyewe namna Timoteo alivyojionyesha kwamba anastahili, kwa maana alitumika kazi ya kueleza Habari Njema pamoja nami kama vile mwana anavyotumika na baba yake.
Sisi ndio wenye kutahiriwa kwa kweli, maana tunamwabudu Mungu kwa uongozi wa Roho wake na kujivuna kwa ajili ya Yesu Kristo. Sisi hatuweki tumaini letu katika mambo ya kimwili.
Ni kwa hiyo nimewekwa kuwa mujumbe na mutume kwa kuwafundisha watu wa mataifa mengine kusudi wapate kumwamini Mungu na kutambua ukweli. Mimi ninasema ukweli wala si uongo.
Ninamushukuru Mungu ambaye ninamutumikia kwa zamiri safi kama vile babu zangu walivyofanya, ninapokukumbuka siku zote katika maombi yangu usiku na muchana.