Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Walawi 9:4 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

4 ngombe dume mumoja na kondoo dume mumoja kwa ajili ya sadaka ya amani, wamutolee Yawe sadaka pamoja na sadaka ya unga uliochanganywa na mafuta kwa maana leo Yawe atawatokea.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Walawi 9:4
18 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Wakati Haruni alipokuwa akizungumuza na Waisraeli wote pamoja, watu wote wakaangalia kule katika jangwa na mara moja utukufu wa Yawe ukaonekana katika mawingu.


wakuwe tayari kwa kesho kutwa, maana siku hiyo ya tatu mimi Yawe nitashuka juu ya mulima Sinai mbele ya watu wote.


Utukufu wa Yawe ukatua juu ya mulima Sinai na wingu likafunika mulima kwa muda wa siku sita. Siku ya saba Mungu akamwita Musa kutoka katikati ya lile wingu.


Hapo ndipo nitakapokutana na Waisraeli na utukufu wangu utapafanya pawe patakatifu.


Utukufu wa Mungu wa Israeli ulitokea upande wa mashariki. Pamoja nao kulikuwa mushindo wa kuja kwake kama mushindo wa maji mengi, inchi ilingaa kwa utukufu wake.


Kisha siku hizo saba, tokea siku ya nane na kuendelea, makuhani watatoa sadaka zenu za kuteketezwa na sadaka zenu za amani. Nami nitawakubali. –Ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe.


Mutu yeyote akileta sadaka ya ngano kwa Yawe, sadaka hiyo ikuwe ya unga laini. Atautia mafuta na ubani.


Kama mutu anatoa sadaka ya amani na sadaka yake ni ngombe dume au dike, nyama huyo asikuwe na kilema mbele yangu.


Halafu Musa na Haruni wakaingia ndani ya hema la mukutano; walipotoka wakawabariki watu, nao utukufu wa Yawe ukaonekana kwa watu wote.


Uwaambie Waisraeli watwae beberu mumoja kwa ajili ya sadaka ya zambi, na mwana-ngombe mumoja na mwana-kondoo mumoja wote wa umri wa mwaka mumoja na wasiokuwa na kilema kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa,


Waisraeli wakaleta vyote hivyo mbele ya hema la mukutano kama vile Musa alivyowaamuru na wote pamoja wakaenda kusimama mbele ya Yawe.


Musa akawaambia: Hili ndilo jambo ambalo Yawe aliwaamuru mulifanye kusudi utukufu wake uonekane kwenu.


Lakini wengine wote pamoja wakatishia kuwapiga mawe. Kwa rafla, utukufu wa Yawe ukatokea juu ya hema la mukutano, mbele ya watu wote wa Israeli.


Naye Kora akawakusanya watu wote pamoja, wakasimama mbele ya Musa na Haruni ambao walikuwa kwenye mulango wa hema la mukutano. Halafu utukufu wa Yawe ukawatokea watu wote.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ