Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Walawi 9:22 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

22 Haruni alipomaliza kutolea sadaka zote: sadaka kwa ajili ya zambi, sadaka za kuteketezwa na sadaka za amani, akawainulia watu mikono, akawabariki, kisha akashuka chini.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Walawi 9:22
16 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Alisimama, akawabariki Waisraeli wote waliokuwa wamekusanyika pale, akisema kwa sauti kubwa:


Wana wa Amuramu walikuwa: Haruni na Musa. Haruni alichaguliwa kwa kazi inayoelekea vitu vitakatifu kabisa, hata wazao wake siku zote wafukizie ubani mbele ya Yawe, wakimutumikia na kuwabariki watu katika jina la Yawe milele.


Kisha Solomono akageukia mukutano wote wa watu wa Israeli wakiwa wanasimama akawabariki.


Jina la mufalme litukuzwe siku zote; utukufu wake udumu muda wote jua litakapokuwa. Kwake mataifa yote yabarikiwe; watu wote wamwite mwenye heri!


Musa akachunguza kila kitu, akaona kwamba walikuwa wamefanya kila kitu kama vile Yawe alivyoamuru. Hivyo Musa akawabariki.


Kisha akawakumbatia watoto wale, akaweka mikono juu yao na kuwabariki.


Kisha Yesu akatoka nao katika muji na kwenda karibu na kijiji cha Betania na pale akainua mikono yake juu na kuwabariki.


Hivi Mungu alimutuma mutumishi wake kwa ajili yenu kwanza, kusudi awabariki ninyi, akimugeuza kila mumoja wenu toka katika njia zake mbaya.”


Wakati huo, Yawe akachagua watu wa kabila la Lawi wakuwe wanabeba Sanduku la Agano la Yawe, wamutumikie kama vile makuhani na kubariki watu kwa jina lake hata hivi leo.


Nao makuhani wa ukoo wa Lawi sharti wakuwe pale. Yawe, Mungu wenu, aliwachagua wamutumikie na kubariki kwa jina lake. Wao vilevile ndio wenye mamlaka ya kuamua magomvi na maneno juu ya kuumizana.


Musirudishiane mabaya kwa mabaya au matusi kwa matusi, lakini muombeane baraka, kwa sababu Mungu aliahidi kuwabariki ninyi wakati alipowaita kumufuata.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ