21 Lakini vile vilali na ule muguu wa nyuma wa kuume, Haruni akafanya navyo kitambulisho cha kumutolea Yawe, kama vile Musa alivyoamuru.
Vyote hivi utavipatia Haruni na wana wake nao wataviinua juu kuwa kitambulisho cha kunitolea sadaka mimi Yawe.
Aliniambia: Wewe ni mutumishi wangu; kwa njia yako, ee Israeli, watu watanitukuza.
Mafuta ya nyama yoyote aliyekufa mwenyewe au ya nyama aliyeuawa na nyama wa pori yanaweza kuwekwa kwa matumizi mengine, lakini musiyakule.
Tena, musikule damu yoyote, ikuwe ya ndege au ya nyama pahali popote munapoishi.
wakayaweka juu ya vilali, naye akaviteketeza kwenye mazabahu.
Mara moja kukaonekana kundi kubwa la wamalaika kutoka mbinguni wakiwa pamoja na yule malaika, wakimutukuza Mungu na kusema:
Yule anayehubiri, anapaswa kutoa ujumbe wa Mungu. Na yule anayetumika, atumike kwa kadiri ya nguvu alizopewa na Mungu, kusudi Mungu atukuzwe katika mambo yote kwa njia ya Yesu Kristo anayekuwa mwenye utukufu na uwezo kwa milele na milele. Amina.