Kisha kusafisha matumbotumbo na miguu kwa maji, Musa akaviteketeza vyote juu ya mazabahu pamoja na sehemu zingine za huyo kondoo kama sadaka ya kuteketezwa. Hiyo ni sadaka inayotolewa kwa moto, yenye harufu ya kumupendeza Yawe. Musa akafanya kama vile alivyoamuriwa na Yawe.
Kisha, Haruni akaleta mbele sadaka ya watu. Akatwaa mbuzi wa sadaka ya watu kwa ajili ya zambi, akamuchinja na kumutoa sadaka kwa ajili ya zambi, kama vile alivyofanya kwa yule wa kwanza.