13 Kisha wakamuletea sadaka ya kuteketezwa, kipande kimojakimoja, na kichwa, naye akaviteketeza juu ya mazabahu.
Atamushika mabawa na kumupasua, lakini asimwachanishe vipande viwili. Kisha, kuhani atamuteketeza kwenye mazabahu, juu ya kuni. Hiyo ni sadaka ya kuteketezwa kwa moto yenye harufu nzuri ya kumupendeza Yawe.
Kisha makuhani hao watatwaa vile vipande vya nyama, kichwa na mafuta, na kuviweka juu ya kuni juu ya mazabahu.
Kisha Haruni akamuchinja nyama wa sadaka ya kuteketezwa. Wana wake wakamuletea damu, naye akainyunyizia mazabahu pande zote.
Akasafisha matumbotumbo na vikanyagio na kuviteketeza pamoja na ile sadaka ya kuteketezwa kwenye mazabahu.