Haruni akamwambia Musa: Angalia, leo wametolea sadaka yao ya kuondoa zambi na sadaka ya kuteketezwa mbele ya Yawe; hata hivyo mambo haya yamenipata! Tena kama ningekula ile sadaka kwa ajili ya zambi hivi leo, ingekubalika mbele ya Yawe?
Wana wake wakamuletea damu, naye akachovya kidole chake katika damu hiyo na kuipakaa kwenye pembe za mazabahu. Damu iliyobakia akaimwanga kwenye tako la mazabahu.
Muishi katika upendo kama vile Kristo alivyotupenda na kutoa maisha yake kwa ajili yetu kama vile matoleo na sadaka ya kuteketezwa kwa moto yenye harufu nzuri inayomupendeza Mungu.