Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Walawi 8:7 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

7 Kisha akamuvalisha Haruni koti na kuifunga kwa mukaba, akamuvalisha kanzu, akamuvalisha kizibao na kukifunga kwenye kiuno chake kwa mukaba uliofumwa kwa ufundi.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Walawi 8:7
12 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Utamushonea ndugu yako Haruni nguo takatifu kusudi apate kuonekana mwenye utukufu na muzuri.


Uwaambie wamutengenezee vitu hivi: kifuko cha kifua, kizibao, kanzu, na ingine yenye kupambwa vizuri, kofia na mukaba. Ndugu yako Haruni na wana wake watavaa nguo zile kusudi wanitumikie kama vile makuhani.


Watatengeneza kizibao cha kuhani kwa nyuzi za zahabu na sufu ya rangi ya samawi, zambarau na nyekundu, na kitani safi iliyosokotwa, na kupambwa vizuri.


Kisha utatwaa zile nguo za kikuhani umuvalishe Haruni: koti, kanzu, kizibao, kifuko cha kifua, na kumufunga ule mukaba uliofumwa kwa ufundi.


Nitafurahi sana kwa sababu ya Yawe, nafsi yangu itashangilia kwa sababu ya Mungu wangu. Maana amenivalisha nguo ya wokovu, amenifunika kanzu ya haki, kama bwana arusi anavyojipamba kwa shada la maua, kama bibi arusi anavyojipamba kwa ushanga wake.


na kuwapa wale wanaoomboleza katika Sayuni taji la maua pahali pa majivu juu ya kichwa, mafuta ya kuangarisha kwa furaha pahali pa maombolezo, nguo ya sifa pahali pa moyo muzito. Nao wataitwa miti ya mialo ya haki, Yawe aliyopanda kuonyesha utukufu wake.


Makuhani ambao watakuwa wakitumika katika Pahali Patakatifu, wanapotaka kwenda kwenye kiwanja cha inje, ni lazima waache humo nguo zao walizovaa walipokuwa wanatumika mbele ya Yawe kwa sababu nguo hizo ni takatifu. Ni lazima wavae nguo zingine mbele ya kutoka inje ambako watu wanakusanyika.


Lakini Bwana Yesu akuwe kama vile silaha munayobeba, musijiachilie kuvutwa na hali yenu ya kimwili hata mutimize tamaa zake.


kuhesabiwa haki na Mungu kunapatikana kwa njia ya imani katika Yesu Kristo kwa wote wanaoamini, kwa maana hakuna tofauti yoyote kati yao,


Hivi, ninyi wote mulioungana na Yesu Kristo, kwa njia ya kubatizwa, ni kama vile mumevaa Kristo.


Kati ya makabila yote ya Israeli nilimuchagua Haruni na jamaa yake kuwa makuhani wangu, wanitumikie kwenye mazabahu, wafukize ubani na kuvaa kizibao mbele yangu. Nikaipatia jamaa ya babu yako sadaka zangu ambazo Waisraeli walinitolea kwa moto.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ