Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Walawi 8:4 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

4 Musa akafanya kama vile alivyoamuriwa na Yawe. Akakusanya Waisraeli wote pamoja mbele ya mulango wa hema la mukutano.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Walawi 8:4
19 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Kwa kutumia sufu ya rangi ya samawi, zambarau na nyekundu walifuma nguo za kuvaa wakati wa kutumika katika Pahali Patakatifu. Walimushonea Haruni nguo takatifu kama vile Yawe alivyomwamuru Musa.


Wakafunga kifuko cha kifua kwenye kizibao kwa kufunganisha pete zake na kizibao kwa kamba ya rangi ya samawi, kusudi kifuko hicho kisiregee lakini kiikalie ule mukaba uliofumwa kwa ufundi, kama vile Yawe alivyomwamuru Musa.


Hivyo, kengele na komamanga vilifuatana kuzunguka upindo wa koti hilo, kama vile Yawe alivyomwamuru Musa.


na mikaba ya kitani safi iliyosokotwa kwa sufu ya rangi ya samawi, ya zambarau na nyekundu na kupambwa vizuri, kama vile Yawe alivyomwamuru Musa.


Mukaba uliofumwa kwa ufundi juu yake kwa kuifunga ulikuwa kitu kimoja na kizibao hicho, na ulitengenezwa kwa vitu hivyohivyo: zahabu, sufu ya samawi, zambarau na nyekundu, na kitani safi iliyosokotwa, kama vile Yawe alivyomwamuru Musa.


Wakaweka mawe yale juu ya mikaba ya mabega za kila kizibao kuwa ukumbusho wa makabila kumi na mawili ya Israeli, kama vile Yawe alivyomwamuru Musa.


Kisha Musa akawaleta wana wa Haruni akawavalisha koti na kuwafunga mikaba kwenye viuno, na kuwavalisha kofia kama vile alivyoamuriwa na Yawe.


Lakini nyama ya ngombe huyo, ngozi yake na mavi yake, akaviteketeza kwa moto inje ya kambi kama vile alivyoamuriwa na Yawe.


Kisha Musa akatwaa kile kilali na kufanya kitambulisho cha kumutolea Yawe. Sehemu hiyo ya yule kondoo dume wa utakaso ni mali ya Musa kama vile alivyoamuriwa na Yawe.


Kisha, ukusanye Waisraeli wote pamoja mbele ya mulango wa hema la mukutano.


Mutabaki kwenye mulango wa hema la mukutano usiku na muchana kwa muda wa siku saba, mukifanya mambo Yawe aliyoamuru, kama sivyo mutakufa. Ndivyo nilivyoamuriwa na Yawe.


Musa akawaambia: Hili ndilo jambo ambalo Yawe ameamuru lifanyike.


Halafu akamuvalisha Haruni kofia na upande wa mbele wa Kofia hiyo akaweka pambo la zahabu, taji takatifu, kama vile Yawe alivyomwamuru.


Muwafundishe kutii maneno yote niliyowaagiza. Na mujue kwamba mimi ni pamoja nanyi siku zote hata mwisho wa dunia.”


Kwa maana haya ndiyo mafundisho niliyopokea kutoka kwa Bwana, nami niliyotoa kwenu: katika usiku ule Bwana Yesu alipotolewa, alitwaa mukate,


Kwanza nimewatolea mafundisho haya ambayo mimi mwenyewe nilipokea: Kristo alikufa kwa sababu ya zambi zetu kama vile Maandiko Matakatifu yanavyosema.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ