Kwa hiyo, Daudi akawakusanya Waisraeli wote katika inchi, tokea kwenye kijito cha Sihori kinachokuwa Misri, mpaka kwenye kiingilio cha Hamati kwa kulileta Sanduku la Agano toka Kiriati-Yearimu.
Kila mutu aliyehuzuria alifurahi sana. Watu wote wa Yuda, makuhani na Walawi, wakaaji wa Yerusalema waliohuzuria, wageni waliotoka inje ya Yerusalema na wale walioishi katika inchi ya Yuda, wote walifurahi sana.
Basi mufalme Solomono akawakusanya kule Yerusalema wazee na viongozi wote wa makabila wa ukoo za Waisraeli kusudi waondoe Sanduku la Agano la Yawe kutoka katika muji wa Daudi, ni kusema Sayuni.
Kisha watu wote, kwa nia moja, wakakusanyika katika Yerusalema kwenye kiwanja kinachokuwa karibu na Mulango wa Maji. Wakamwambia Ezra, mwandishi, alete kitabu cha sheria ya Musa ambayo Yawe aliwapa watu wa Israeli.
Utwae Haruni na wana wake na zile nguo takatifu, mafuta ya kupakaa, ngombe wa sadaka kwa ajili ya zambi, kondoo dume wawili, na kitunga cha mikate isiyotiwa chachu.
Twaa ile fimbo yako, kisha wewe na ndugu yako Haruni mukusanye watu wote pamoja. Halafu, mbele ya macho yao, uambie jiwe linalokuwa mbele ya macho yao litoe maji yake. Utawatoshea maji ndani ya jiwe watu wote na mifugo yao waweze kunywa.